DK SALIM ASEMA: SINA MPANGO WA KUGOMBEA URAIS MWAKA 2015!!

Kufuatia uchaguzi mkuu wa ujao wa mwaka 2015 Dr Salim Ahmed Salim amefunguka na kusema kuwa wapiga kura wawe makini katika uchaguzi ujao ili kupata viongozi bora.

 “Ni vizuri viongozi wakaandaliwa, isiwe mtu anaibuka tu anagawa hela halafu anashinda. Anatakiwa mtu atakayeweza kushughulikia matatizo ya Watanzania. Watanzania ni wapole na wavumilivu lakini wanazungumza. Hivyo anahitajika kiongozi atakayesikiliza mahitaji yao na kutoa suluhisho, si kutoa ahadi za uongo,” Dk Salim Ahmed Salim  

“Hapa sizungumzii viongozi wa CCM au wa Chadema au chama kingine, nazungumzia viongozi wa nchi watakaoweza kufanyia kazi matatizo ya Watanzania.

“Ni vizuri viongozi wakaandaliwa, isiwe mtu anaibuka tu anagawa hela halafu anashinda. Anatakiwa mtu atakayeweza kushughulikia matatizo hayo. 

Watanzania ni wapole na wavumilivu lakini wanazungumza. Hivyo anahitajika kiongozi atakayesikiliza mahitaji yao na kutoa suluhisho, si kutoa ahadi za uongo,” alisema.

 Dk Salim alisema katika kipindi hiki, anahitajika kiongozi atakayekuwa juu ya tofauti za kisiasa, kidini, asili.
“Unajua hapa nchini kama ilivyo mahali pengine, ukiingiza mgawanyiko wa kidini wakati familia nyingi zina watu wa dini tofauti, wote wataathirika.”
Akizungumzia tatizo la rushwa, Dk Salim alisema ni kubwa na kadri linavyoongezeka, linakuwa adui wa uwajibikaji, demokrasia.
Alisema katika enzi za utumishi wake nje ya nchi, alikuwa akiona rushwa ilivyokithiri katika nchi mbalimbali, lakini hapa nyumbani pakiwa salama hadi akawa anasema Tanzania ina bahati, kauli ambayo hawezi kuisema sasa.
Dk Salim alibainisha kuwa uongozi unaoingia madarakani kwa rushwa hauwezi kuwa mzuri kwa nchi na athari zake zinaonekana hadi ngazi ya chini katika huduma za jamii kama mahakamani, polisi na hospitalini.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment