Wanachama na Viongozi wa Chadema wakiwemo wa Baraza Kuu la chama hicho,
wakipiga kwata kuelekea Ofisi za Msajili wa Vyama vya Siasa, jijini Dar
es Salaam, leo kupeleka barua ya kumuomba Msajili huyo wa vyama,
kuwataka viongozi wa ngazi ya juu wa Chadema kuzingatia Katiba ikiwemo
kuitisha kikao cha Baraza Kuu na kuzingatia matumizi bora ya fedha za
Chama.
Mjumbe wa Baraza Kuu Chadema ambaye pia ni Mwenyekiti wa chama hicho
wilaya ya Temeke Joseph Yona (kushoto) akiongoza wenzake kuingia Ofisi
ya Msajili wa Vyama leo kuwashitaki viongozi wa ngazi ya juu wa chama
hicho kwa kudaiwa kutotekeleza Demokrasia na kufuata Katiba ndani ya
Chama
Yona akisaini kitabu cha wageni kwenye kwenye mapokezi ya Ofisi ya
Msajili wa Vyama Jijini Dar es Salaam, alipowasili ya ujumbe wake. Kulia
kwa Yona ni Mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Kaliua mkoani Tabora ambaye
ni Mjumbe wa Baraza Kuu na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Chadema, Jorum Mbogo
Naibu Msajili wa vyama vya Siasa Nchini akimkaribisha Yona na msafara wake.
Wanachama waliofuatana na wajumbe wa Baraza Kuu Chadema wakisubiri
kuwasilisha barua yao kwa Mkuu wa Masijala wa Ofisi ya Msajili wa vyama.
0 comments:
Post a Comment