Baada ya kipindi cha miaka kumi jeshi la Ujerumani Bundeswehr Jumapili(06.10.2013) limekamilisha jukumu lake kaskazini mwa Afghanistan kwa kukabidhi rasmi mamlaka ya kambi yao ya Kunduz kwa vikosi vya Afghanistan.
Waziri huyo amesema juu ya kwamba jeshi la Ujerumani linaondoka katika jimbo hilo amesisitiza kwamba katu hawatolisahao kwa kuwa lina umuhimu mkubwa wa kiishara kwa jeshi la Ujerumani. Amesema Kunduz ni mahala ambapo imelishughulisha jeshi la Ujerumani kuliko mahala popote pale,hapo walijenga na kupigana,walilia na kujifariji,waliuwa na kuuliwa. de Maiziere amesema "Kunduz daima itakuwa sehemu ya kumbukumbu yetu ya pamoja."
@DW
POSTED BY:www.info@dirayetu.blogspot.com
0 comments:
Post a Comment