MVUTANO WA KIWANJA MANISPAA YA MOSHI WACHUKUA SURA MPYA!!


 

Mvutano umeibuka katika Mji wa Moshi utata ukiwa nani hasa ni mmiliki halali wa kiwanja chenye hati namba 10660 ambacho Manispaa ya Moshi imekitumia kwa miaka 40 sasa.
Mgogoro huo uliozua sintofahamu wiki iliyopita, ulisababisha madiwani wanaotokana Chadema ambao ndiyo wengi, kususia kikao cha Baraza la Madiwani kilichokuwa kijadili bajeti ya manispaa hiyo kwa mwaka 2015/2016.
Wakiongozwa na Meya wa Manispaa ya Moshi, Jaffar Michael, madiwani hao walisusia kikao hicho wakipinga kile walichodai ni “mpango” mahususi unaofanywa na vigogo wa Serikali kusaidia kuporwa eneo hilo.
Kitendo cha madiwani hao wa Chadema ambao ndiyo wanaoongoza Baraza la Madiwani Manispaa ya Moshi kususia kikao hicho, kumeibua maswali mengi kwa wananchi, wakitaka kujua ukweli halisi wa mmiliki wa kiwanja hicho.
Kiwanja hicho kipo katikati ya mji kwenye eneo la kibiashara kimepakana na jengo la makao makuu ya polisi Mkoa Kilimanjaro pia ndipo zilipo ofisi za Serikali za Kata ya Mawenzi ya mjini Moshi.
Ni kiwanja hicho hicho ambacho mwaka 2012, kilianishwa kama eneo la uwekezaji na halmashauri ikalitangaza rasmi katika kikao cha Kanda ya Kaskazini kilichofanyika mkoani Tanga ili kuvutia wawekezaji.
Mbali na kiwanja hicho kuwa na jengo la ofisi ya Serikali Kata ya Mawenzi kwa miaka 40 mfululizo, kuna maduka ambayo wapangaji wake wanalipa kodi zao moja kwa moja kwa halmashauri husika.
Hata hivyo, wakati Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ikiwa katika mchakato wa kutafuta hati ya kumiliki kiwanja hicho, imejitokeza Taasisi ya Mawenzi Sports Club (MSC), inayodai kulimiliki eneo hilo.
Tayari Meya wa Manispaa ya Moshi, Jaffar Michael na madiwani wake, wameweka kizuizi kisheria ili kuzuia mtu yoyote au taasisi kufanya uhamisho wa umiliki wa kiwanja hicho.
Wakati hayo yakiendelea, leo Januari 26, madiwani wa halmashauri hiyo wanakutana katika kikao maalumu cha baraza lao kwa lengo la kujadili ajenda moja tu nayo ni kuhusu kiwanja cha Mawenzi, hasa; nani ni mmiliki halali wa kiwanja?
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment