Waziri Nahodha atembelea ujenzi wa nyumba za Wanajeshi Dar

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Shamsi Vuai Nahodha akiangalia ubora wa matofali yanayotumika kujenga nyumba za wanajeshi kwa kulivunja moja wapo ya matofari yanayofyatuliwa na Kampuni ya Shanghai Construction Group Ltd DSC_0307Waziri wa Ulinzi na JKT Mhe. Shamsi Vuai  Nahodha akiwa katika Kambi ya Kigamboni kujionea ujenzi wa nyumba za wanajeshi  ambazo ziko katika hatua ya msingi DSC_0340Moja wapo ya ghorofa ambayo inajengwa katika kambi ya Lugalo DSC_0349Mafundi wakiwa  kazin ni katika kambi ya Lugalo.

   
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe Shamsi Vuai Nahodha amefanya ziara kwa lengo la kujionea mradi wa ujenzi wa nyumba 6064 za JWTZ unaofanywa na Kampuni ya China Construction Group Ltd toka nchini China. Ziara hiyo ya Waziri ilihusisha miradi inayoendelea kujengwa katika Kambi ya Kigamboni na Lugalo, ikiwa ni utekelezaji wa awamu ya kwanza ya zabuni ya ujenzi unaotarajiwa kuwa umekamilika mwezi Agosti mwaka 2014.
Katika ziara hiyo Waziri Nahodha alianza kwa kutembelea kambi ya Kigamboni yenye nyumba 38 ambapo mpaka sasa ujenzi upo katika hatua ya awali ya kutayarisha msingi huku watendaji wakionesha kuwa na kasi kwani vitendea kazi vyote vinapatikana eneo la ujenzi. 
Akiwa ziarani Waziri Nahodha alihimiza ujenzi ufanyike kwa wakati kwa kuzingatia mkataba na michoro inavyoelekeza na sio vinginevyo. Waziri alisema kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wakandarasi kukiuka makubaliano ya awali ambapo aliwataka wasimamizi kutoka Wizarani kuhakikisha kuwa mikataba na michoro inafuatwa.
Akiwa katika Kambi ya LugaloMhe. Waziri alijionea ujenzi huo ukiwa katika hatua ya ghorofa ya pili kwa baadhi ya nyumba na nyingine zikiwa usawa wa msingi, jambo ambalo lilimpa matumaini makubwa kuwa kampuni hii inakamilisha ujenzi huo kwa Kanda ya Dar es Salaam mwezi Agosti 2013.

Ujenzi huu unajumuisha kambi za Gongolamboto, Air Wing, Kigamboni na Lugalo ambapo mradi huu unalenga kujenga nyumba 6,064 kwa jeshi zima na ni mradi unaotarajiwa kupunguza adha ya makazi kwa wanajeshi kuishi uraiani jambo ambalo sio utaratibu mzuri kijeshi. Ziara ya Mhe. Nahodha pia iliambatana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bi. Rose Shelukindo, baadhi ya wakuu wa Idara kutoka Wizara ya Ulinzi na JKT na JWTZ.
Baada ya kumaliza ziara yake alipata wasaa wa kuongea na wawakilishi wa Kampuni ya Shanghai pamoja na usimamizi wa mradi huo na kuwataka kuwa makini katika hatua hii ya awali kwani ndiyo hatua muhimu zaidi katika ujenzi, hususan kwa nyumba hizo za ghorofa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment