WAZIRI 
 Mkuu Mizengo Pinda ametoa wito kwa vyuo vikuu , taasisi za serikali, 
benki  na jamii  kutumia Tovuti   Kuu ya Serikali na Mkongo wa Taifa wa 
Mawasiliano katika kupata huduma mbalimbali za serikali ili 
  kurahisisha  mawasiliano kwa gharama nafuu.
Kauli
 hiyo imetolewa jana jioni na Waziri Mkuu, mheshimiwa  Pinda wakati 
akizindua Tovuti Kuu ya Serikali katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu 
Julius K. Nyerere  jijini Dares Salaam mara baada ya  kutembelea   ofisi
 ya Wakala ya Serikali  Mtandao (eGA) na Mkongo wa Taifa. 
 Akizungumzia
 kuhusu tovuti hiyo Waziri Mkuu Pinda alisema kitu muhimu ambacho mtu 
yoyote kuweza kupata taarifa  anazozihitaji mfano vile masuala ya kilimo
 au  kuomba uraia wa Tanzania. Hivyo lengo lake ni kuisadia Serikali 
kufanya kazi kiutalaam.
“
 Kwa hiyo ni mambo yanayoifanya nchi kwenda kwa wakati. Tumeanzisha 
matumizi ya  tovuti hii kwa  sababu mahitaji yake  katika soko ni 
makubwa,”  alisema  Waziri Mkuu Pinda.
 Akizungumzia
 kuhusu  mkongo huo alisema  moja ya changamoto iliyopo  matumizi yake  
bado ni  madogo, kwani  yako  chini  ya asilimia tano , hivyo kuna 
umuhimu wa kuongeza kasi ya matumizi.
 Alisema  Serikali itaendelea  kukabiliana  na changamoto za kiusalama katika masuala hayo.
Kwa
 upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais , Menejimenti ya Utumishi wa 
Umma, Celina Kombani aliwataka wanafunzi na vijana kubadili  mtazamo kwa
 kutumia mitandao ya kijamii kwa mambo yasiyofaa badala yake  watumie 
tovuti hiyo ili kuweza kuelewa  historia ya nchi ,sheria na mambo 
mengine  mbalimbali.
 Aliongeza  kuwa tovuti hiyo inarahisisha utoaji wa huduma za Serikali kwa wananchi , pia na kuongeza uwajibikaji.
 Kwa
 upande wake  Mtendaji Mkuu wa  wakala huo, Dk. Jabiri  Bakari  alisema 
ina sehemu sita ambazo ni wananchi, Serikali,Taifaletu, Biashara, Sekta 
muhimu na Mambo ya Nje.
  Aliishauri Serikali kuviwezesha vitengo vya mawasiliano vya Serikali ili kuviwezesha kuweka taarifa sahihi kwa wakati.
 Aidha
 Jabiri alisema katika wameshaanza kazi ya kuwezesha  taarifa muhimu za 
Serikali  kupatikana kwa njia ya simu na iko kwenye hatua nzuri.
Alizipongeza
 Ofisi mbalimbali zilizowesha uwepo wa tovuti hiyo, ambazo Ofisi ya Rais
 , Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Katibu Mkuu Kiongozi, Wizara ya 
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kupitia Idara ya Habari –MAELEZO 
 na Kamati ya Bunge  ya Sheria ,Katiba na Utawala.
POSTED BY:www.info@dirayetu.blogspot.com  
 
 
0 comments:
Post a Comment