WATAALAMU WATAKIWA KUFUNDISHA WAKULIMA KUTUMIA MBEGU ZA MUDA MFUPI PAMOJA NA KILIMO CHA MATUTA HAI!!




Wataalamu wa kilimo pamoja na Madiwani katika wilaya ya Hai wametakiwa kufundisha wakulima kutumia mbegu za muda mfupi pamoja na kuotesha  kwakutumia matuta.

Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Halimashauri ya Wilaya ya Hai Bw.Clement Zablon Kwayu wakati alipokuwa akifungua kikao cha baraza la Halmashauri ya Hai Mkoani Kilimanjaro.

Bwana Kwayu alisema ni vema wakulima wakahamasishwa kutumia na kuotesha mbegu za muda mfupi ili waweze kupata chakula chakutosha  kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha hivi sasa.

Aidha aliendelea kusema kuwa upo umuhimu wakuwafundisha wakulima kutumia kilimo chakuotesha kwa matuta kutokana  kunyesha mvua  kubwa kwa muda mfupi na kuhamisha udongo na mbegu.

Vile vile amesema wenye matrecta wanalima kwakulenga kupata pesa hivyo ni vizuri wakulima wakashauriwa na kupewa  umuhimu wakubadilisha mwelekeo wakulima mashamba tofauti na wanavyolima kila mwaka.

 ‘’kilimo kinachotumiwa na wenye matrecta siyo cha kitaalamu ndiyo maana inaponyesha mvua kidogo udongo na mbegu vinahamishwa’’ alisema Bwana Kwayu.

Hata hivyo Bwana Kwayu aliendelea kusema kuwa kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa inayosababisha mvua kupungua ni vizuri wakulima wakapewa utaalamu wakuvuna maji ya mvua kwa matumizi ya baadae kwenye kilimo cha umwagiliaji.

Kikao hicho cha baraza la Halmashauri ya Wilaya kilikutana kujadili mambo mbalimbali yakiwepo mgogoro wa ardhi za wananchi miatatu kumi na saba zilizochukuliwa mwaka elfu moja mia tisa na sabini na tano kwaajili yakupanua na kujenga makao makuu ya wilaya pia kupisha rasmu ya katiba ya halmashauri hiyo.
Chanzo:Emanuel O.Ndanshau
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment