Majaji wa Shindano la Kusaka la Vipaji vya Uigizaji Tanzania lijulikanalo kama 
Tanzania Movie Talents wakijadiliana jambo wakati wa Zoezi la kusaka 
vipaji vya uigizaji kuingia Hatua ya pili kwa washiriki waliofanikiwa 
kupita kwenye mchujo.Kulia ni Single Mtambalike (Rich Rich), Ivon Chery 
(Monalisa) na Roy Sarungi.
Washiriki waliofanikiwa kuingia kwenye hatua ya pili wakifanyiwa usaili kwaajili ya hatua ya pili sasa
Muongozaji wa 
Mradi wa Shindano la Kusaka Vipaji vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo 
kama Tanzania Movie Talents, Bw Stanford Kihole (kulia) akitoa maelekezo
 kwa washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya pili katika mashindano ya 
kusaka vipaji vya uigizaji Tanzania likiwa limeaingia hatua ya pili 
Mkoani Mwanza
Baadhi ya 
Washiriki waliofanikiwa Kuingia katika Hatua ya Pili ya Shindano la 
Kusaka Vipaji vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie 
Talents wakiwa makini kusikiliza maelekezo juu ya hatua ya pili 
waliofanikiwa kuingia.
 Baadhi ya 
washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya pili wakiwa mbele ya majaji 
kwaajili ya kupewa maelekezo ambapo washiriki watapewa muswada (script) 
kwaajili ya hatua ya pili ambapo wataingia wawili wawili na kuanza 
kuonyesha vipaji vyao.
Kikosi Kazi 
kikiendelea kurekodi matukio yanayoendelea katika Shindano la Kusaka 
Vipaji Vya Kuigiza Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents 
linaloendelea kufanyika Kanda ya Ziwa, Mkoani Mwanza.
 Baadhi
 ya washiriki waliofanikiwa kuingia hatua ya pili katika Mashindano ya 
Kusaka Vipaji vya Uigizaji Tanzania lijulikanalo kama Tanzania Movie 
Talents wakiwa makini katika kupitia muswada (script) waliopewa na 
majaji ili waweze kusoma na baadae kuingia mbele ya majaji na kuonyesha 
vipaji vyao kutokana na muswada (script) waliopewa.
0 comments:
Post a Comment