SERIKALI YAWAPONGEZA WADAU WA SANAA ZA MAONESHO!!

ZT-3 

 Serikali imewapongeza wahisani wa maendeleo kwa kufadhili na kukuza sanaa ambao wamekuwa wachangiaji muhimu wa kuendeleza na kukuza uchumi na kupunguza umasikini miongoni mwa wasanii na Taifa kwa ujumla.
 
Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga alipokuwa akizindua programu ya “kujenga fursa kwa wasanii wa sanaa za maonyesho iliyoratibiwa na asasi isiyo ya Kiserikali ijulikanayo kwa jina la Nafasi Arts space hivi karibuni jijini Dar es Salaam.
 
Sihaba amesema kuwa kuanzishwa kwa dhana ya Programu hii kunatoa fursa ya kujipatia kipato na kuongeza ujuzi ambao utapanua wigo wa ubunifu kwa wasanii na kuongeza mahusiano baina yao na wasanii wengine, ikiwemo kupanua soko la bidhaa zao.
 
“Nachukua fursa hii kuwashukuru na kuwapongeza kwa dhati Nafasi Art Space kwa uamuzi huu mahususi mlioufanya wa kuratibu uanzishwaji wa Programu ya kuibua fursa kwa wasanii wa Sanaa za Maonyesho Tanzania.” Alisema Bi. Sihaba
 
Aidha Katibu Mkuu huyo aliongeza kuwa Serikali kwa kushirikiana na wadau wa sanaa imekuwa ikifanya juhudi za kutosha kuinua viwango vya sanaa nchini kwa kuanzisha programu za kitaifa na kimataifa.
 
Aidha Bi. Sihaba alisema kuwa programu kama hizi zitasaidia kubadilishana habari, ujuzi, mikakati na ubunifu  miongoni mwa wasanii kitaifa na kimataifa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment