CUF KUADHIMISHA MIAKA 14 YA MAUAJI ZANZIBAR.


 


 CHAMA cha Wananchi (CUF), kitaadhimisha kumbukumbu ya miaka 14 tangu kufanyika kwa mauaji ya wananchi wa Zanzibar na kuteswa kwa wananchi Tanzania Bara.

Taarifa hiyo iliyotolewa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam na Naibu Mkurugenzi Habari na Uenezi, Abdul Kambaya, imeeleza wakati wa maadhimisho hayo, pia yatafanyika maandamano makubwa yatakayoongozwa na Mwenyekkiti wa CUF Taifa Prof. Ibrahim Lipumba pamoja na viongozi wa taasisi mbalimbali.

Maandamano hayo yataanzia viwanja vya ofisi ya CUF Temeke na kuishia kwa Mkutano wa hadhara kwenye viwanja vya Zakhiem Mbagala. Kaulimbiu ya mwaka huu ni 'Bila Uchaguzi huru na wa Haki 2015 Taifa linaweza likarudia historia ya 2001'.

Alisema ikiwa ni sehemu ya kumbukumbu hiyo bendera zote za CUF siku ya kesho zitapeperushwa nusu mlingoti ikiwa ni kuomboleza vifo vya wana-CUF na wananchi wengine zaidi ya 70 waliouawa Zanzibar.

Alisema ni sehemu ya kukumbuka ya mateso waliofanyiwa wana-CUF walioandamana Tanzania Bara ikiwemo tukio la kuvunjwa mkono kwa Prof. Ibrahim Lipumba, wakati wa maandamano hayo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, maadhimisho haya ni sehemu ya shughuli za wanaharakati wa demokrasia kutathmini kama taifa la Tanzania linafuata misingi ya Haki na Demokrasia.

Pia ni sehemu ya kupanga mikakati mipya kuhakiksha Tanzania inakuwa na Demokrasia na Uhuru wa kweli inayofuata misingi ya haki za binadamu.

Kila mwaka Chama cha Wananchi (CUF) kimekuwa na utaratibu wa kufanya maadhimisho ya kumbukumbu ya mateso na mauaji yaliyotokea mwaka 2001 Tanzania Bara na Zanzibar.

Mateso na mauaji ya watu hao yalifanywa na vyombo vya usalama baada ya wananchi hasa wanachama wa CUF kuandamana kupinga matokeo batili ya Uchaguzi, Kudai Katiba Mpya,Tume Huru ya Uchaguzi na kudai Daftari la Kudumu la Wapigakura.

Aidha katika kuadhimisha siku hiyo, Chama kimepanga kufanya maandamano.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment