KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI ZAMITAA YAMTAKA MASABURI KUJIUZULU!!


 


KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Rajab Mbarouk Mohamed, imemtaka Meya wa Jiji la Dar es Salaam Dkt.Didas Masaburi, kujiuzulu wadhifa huo kabla ya hajawasilisha ushahidi bungeni unaoonesha alisaini kuuzwa kwa hisa za Shirika la Usafiri Mkoa wa Dar es Salaam (UDA).

Akizungumza Dar es Salaam katika Mkutano wa hadhara uliondaliwa na Jumuiya ya Vijana ya Chama cha Wananchi (JUVICUF), Mwenyekiti wa LAAC Rajab Mohamed Mbarouk, alisema Meya huyo aliihakikishia Kamati hiyo kuwa endapo itabainika yeye alisaini uuzwaji wa hisa za UDA kwenda kwa Kampuni ya Simon Group, basi atajiuzulu.

Alisema ana ushahidi kamili kuwa Jiji lilifanya hivyo katika uuzwaji wa hisa hizo, lakini haikuambulia hata shilingi moja kutokana na uuzwaji wa hisa hizo wakati ilitakiwa kulipwa sh.bilioni tano ambapo Meya huyo alimwambia kuwa ikiwa atakuwa na ushahidi kuwa yeye alihusika na kusaini uuzwaji wa hisa hizo basi atajiuzulu.

"Ninasema hivi Siku za Masaburi zinahesabika, Januari 28 mwaka huu nitawasilisha rasmi ushahidi bungeni kuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam amesaini katika uuzwaji wa hisa za UDA kwenda kwa Kampuni ya Simon Group bila jiji kulipwa hata shilingi moja jambo ambalo halikubaliki kwani UDA ni Shirika la Umma, hivyo kama anataka kujiuzulu basi ajiuzulu sasa hivi kabla sijatoa ushahidi bungeni," alisema Mbarouk.

Alisema mbali na hilo lakini pia jiji lilianzisha mradi wa Machinjio ambapo fedha za mradi huo zilikuwa sh. bilioni 1.7 eneo lenye ekari 80 lakini cha ajabu na cha kusikitisha hakuna machinjio yoyote yaliyojengwa na hadi juzi akaunti iliyowekwa fedha hizo ilikuwa na kiasi cha sh.51,000 tu badala ya sh.bilioni 1.7.

Mbarouk ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ole kupitia CUF aliongeza kuwa Sheria inazitaka Halmashauri zote nchini kutenga asilimia 10 ya fedha zao kwa ajili ya Vijana na akinamama, lakini hazitengwi.

Kwa upande wake Katibu wa JUVICUF Wilaya ya Ilala, Abdul Khomein, alisema Serikali ya CCM haina huruma na watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) vifaa ikiwemo dawa kuuzwa kwa bei ghali.

"Sisi walemavu wa ngozi tunaishi kwa mashaka ndani ya nchi hii; lakini Serikali ya CCM inashindwa kushusha hata mafuta ambayo yanasaidia kuwakinga na mionzi ya jua ambayo inauzwa kiasi cha sh.40,000 hali ambayo walemavu hao wengi hawawezi kumudu kununua," alisema Khomein.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment