WAFANYAKAZI KUSUSIA UCHAGUZI MKUU OCTOBA 2015.


 NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGU) Taifa, Kibwana Njaa, ameitaka Serikali kuwalipa wafanyakazi deni lao la sh.biloni 17 ifikapo Julai 31, mwaka huu kinyume chake hawatashiriki Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Kauli hiyo ameitoa jana wakati akizungumza na wanachama wa TALGU ambao wanafanya kazi Halmashauri ya Manispaa ya Songea na Halmashauri ya Songea Vijijini mjini Songea.

Aidha Bw Kibwana Njaa ameyasema hayo kwenye ziara yake ya Mkoani Ruvuma yenye lengo la kujua matatizo ya wanachama wao. Alisema deni hilo la miaka mitano limekuwa likichukuliwa na serikali kwa uzito mdogo.

Alisema wanaamini kuwa Serikali inaweza kulipa deni hilo, lakini inashindikana kwa sababu si kipaumbele chake; hivyo kama haitalipa hadi Julai 31, mwaka huu basi chama hicho kitahamasisha wafanyakazi nchi nzima kuanzia Serikali za mitaa kugomea Uchaguzi Mkuu ujao.

“Ikifikapo Julai 31, kama Serikali haitalipa deni hilo basi tutashiriki mgomo wa kususia uchaguzi, kwani bila kuchukua hatua hiyo kwa nchi hii hatuwezi kufika na viongozi ni wale wale hata huyo rais atakayechaguliwa hatuna imani naye kama hataweza kulipa deni hilo,” alisema Njaa.

Aidha aliwataka wanachama hao kushikamana japokuwa kwa sasa, TALGU bado ina changamoto nyingi ikiwemo kupata mtaji wa fedha kwa ajili ya kuwakopesha wanachama wake kwa riba ndogo, kwani baadhi ya taasisi za fedha zinazowakopesha wafanyakazi zimekuwa si rafiki kutokana na riba.

“Tumeanzisha taasisi ya fedha kwa ajili ya kuwakopesha wanachama wetu kwa sababu tuliona taasisi za fedha zingine si rafiki kwa kuwa zinatoa mkopo kwa wanachama wetu kwa riba kubwa jambo ambalo linasababisha wafanyakazi kuwa na maisha magumu kila siku,” alisema Njaa.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment