MATOKEO YA MECHI YA SIMBA VS MBEYA CITY, TP MAZEMBE VS AZAM FC!!

soccer-start-and-restart-of-play
Mechi kati ya timu ya Simba SC na Mbeya City imemaliza muda mfupi uliopita, Simba wamejikutawakikubali kichapo cha goli 2-1 katika mechi ya ligi kuu soka Tanzania bara iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mabao ya Mbeya City yamefungwa na Hamad Kibopile na Yusuph Abdallah aliyefunga kwa njia ya penalti, wakati goli la Simba limefungwa na Ibrahim Hajib ‘Mido’.
Hata hivyo dakika ya mwisho ya mchezo, Masoud Nassor ‘Cholo’ amekosa mkwaju wa penalti baada ya beki Yusuph kumfanyia madhambi Jonas Mkude katika eneo la hatari.
Hiki ni kipigo cha pili kwa Simba ndani ya uwanja wa Taifa, December 26 mwaka jana walifungwa bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar.
Mechi kati ya timu ya TP Mazembe ya Congo na Azam FC ambayo imemalizika pia muda mfupi uliopita katika Uwanja wa timu ya TP Mazembe ambapo wenyeji hao wameibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment