NECTA YAANZA KUTUMIA GPA KUPANGA MADARAJA!!

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA)limeanza kutumia mfumo wa wastani wa Pointi (GPA) katika upangaji wa madaraja ya ufaulu katika matokeo ya mitihani ya kidato cha nne na sita.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, MKuu wa Idara ya Fedha na Utawala, Daniel Mafie, alisema kwa kutumia mfumo huo itakuwa rahisi hata kwa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) Kufanya udahili kwa wanafunzi.

Alisema kutokana na maoni ya wadau wa elimu, kuanzia mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012, NECTA walianza kutumia mfumo wa viwango visivyobadilika.

"Kwa kutumia mfumo huu wa viwango vya ufaulu vinavyofanana hupangwa ili viwe kipimo cha ufaulu kwa masomo yote kila mwaka, mfumo huu mpya wa viwango vya ufaulu visivyobadilika umewezesha watahiniwa kujua viwango vya alama vinavyotumika kutunuku matokeo," alisema Mafie.

Aliongezea kuwa awali mfumo wa GPA ulikuwa ukitumiwa katika mitihani ya ualimu na mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi(PSLE) pekee na wakati huo madaraja ya ufaulu katika mtihani wa kidato cha nne na sita yalikuwa yakipangwa kwa kutumia mfumo wa jumla ya pointi.

Alisema mfumo wa jumla ya pointi umekuwa ukitumika kuanzia Baraza lilipoanzishwa mwaka 1973 hadi julai 2014. Alisema mfumo wa ufaulu ulioneshwa kwa kutumia madaraja manne, yaani daraja la kwanza, la pili, la tatu na nne.

Hata hivyo, alisema kutokana na maboresho yaliyofanywa, madaraja ya ufaulu katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne 2014 yamepangwa kwa kutumia mfumo wa wastani wa pointi GPA.

Alisema mfumo wa GPA utatumika pia katika matokeo ya mtihani wa kidato cha sita kuanzia mwaka 2015. Vile vile alisema umewezesha kuwepo kwa mfumo wa kutunuku matokeo wa aina moja katika ngazi zote za mafunzo kuanzia elimu ya msingi hadi elimu ya juu. Pia alisema mfumo wa GPA ni rahisi kueleweka kwa wadau wa kada mbalimbali kwa sababu hutoa tafsiri yenye kuonesha mtahiniwa aliye na GPA kubwa ndiye aliye na matokeo mazuri kuliko aliye na GPA ndogo.

Hata hivyo, alisema matokeo yaliyo katika mfumo wa wastani wa pointi kwenye cheti yatarahisisha udahili wa watahiniwa unaofanywa na Tume ya Vyuo Vikuu(TCU) Baraza la Elimu ya Ufundi (NACTE)katika ngazi za juu za Mafunzo.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment