NYAKATI TOFAUTZI ZA KUJIFUNGUA!!

Katika makala zilizopita mengi yaliongelewa kuhusu ujauzito na umuhimu wa mahudhurio ya kliniki. Jambo hili ni sehemu tu ya kile kinachopaswa kufanywa ili uzazi uhesabike kuwa salama.
Ni jambo linalofahamika kwa wengi kuwa ujauzito huchukua takribani miezi tisa.
Katika kipindi hicho kuna wakati mama kuhesabika kuwa amejifungua bila  kujali kwamba kiumbe hicho kiko hai au la. Makala hii itafafanua juu ya jambo hili. Mwezi hautumiki tena siku hizi kujua umri halisi wa mimba kwa kuwa unatofautiana kwa siku. Kinachotumika sasa ni kigezo cha wiki. Wiki haibadiliki huwa ni siku saba.
Kwa kigezo hiki mimba huhesabika kuwa imekamilika iwapo itafikisha umri kati ya wiki 38 na 42. Na ili kufahamu mambo mbalimbali yanatokea wakati wa ujauzito, kipindi cha mimba hugawanywa katika sehemu kuu tatu, kila kimoja kikiwa na wiki 14.

Hapo awali ilihesabiwa kuwa jambo lolote litakalosababisha kiumbe kutoka kati ya wiki ya kwanza  na 28 basi hii itajulikana kuwa mimba imeharibika.
Hii ilitokana na ukweli kwamba haihesabiwi kuwa ni kujifungua kwami ilikuwa nadra sana, kwa kiumbe hicho chenye umri unaokadiriwa wa miezi sana, kuweza kuishi.

Lakini kutokana na maendeleo makubwa ya sayansi kiumbe kinachotoka kikiwa hai na umri wa wiki 24, wastani wa miezi sita, kinaweza kutunzwa na baadae kikakua na kufikia umri wa kawaida.
Hivyo mwanamke alietoa kiumbe hicho sasa huhesabiwa kuwa amejifungua. Jambo hili kwa kiasi kikubwa hutegemeana na huduma za afya ya uzazi katika nchi husika.

Kwa nchi zilizoendelea kuweza kukilea kichanga kilichozaliwa kikiwa na umri wa wiki 24 na kwa kiasi kikubwa bado ni tatizo katika nchi zetu zinazoendelea.

Huduma za kipekee huhitajika ili kiumbe kinachozaliwa katika umri huo kiweze kuishi. Hii ni pamoja na wataalamu, vifaa na vyumba maalumu vya kutunzia vichanga hivi.
Wako ambao hutangulia kufika vituoni kwa ajili ya kujifungua wakati muda wa kufanya hivyo unakuwa haujawadia. Hii huwaletea usumbufu usio wa lazima kwani hulazimika kurudi nyumbani ili kusubiri muda muafaka.
Ni jambo la kawaida kwa mjamzito kupata maumivu kama ya kujifungua kuanzia wiki ya 26 na kuendelea wiki ya 36 lakini haimaanishi hivyo. Pia wapo ambao huchelewa kufika vituoni kwa kutokujua.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment