VYETI VYA KUZALIWA KUTOLEWA KWA WANAFUNZI WA SHULE ZA MSINGI!!

Waziri wa katiba na Sheria Dk Asha-Rose Migiro (katikakati) akikata utepe kuashiria kuzindua mkakati wa usajili na kutoka vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi wa shule za msingi Wilaya ya Kinondoni (Kushsoto) ni Mbunge wa Kindonindoni Iddy Azzan, Mewa wa Manisapa ya Kinondoni Yussuf Mwenda, Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA  Philip saliboko na Mkurugenzi wa Manisapaa ya Kinondoni,  Mhandisi Mussa Natty
Wakala wa Usajili na ufilisi na Udhamini(RITA) imezindua  mkakati wa usajili na kutoa vyeti kwa wanafunzi wa shule za msingi katika Manispaa ya Kinondoni mashuleni lengo likiwa ni kusogeza huduma karibu kwa watanzania.


Akizungumza kwenye uzinduzi huo leo Waziri wa Katiba na Sheria, Dk Asha-Rose Migiro amewaagiza RITA kuhakikisha kuwa wanatoa mafunzo ya kutosha kwa walimu watakaoshiriki katika zoezi la usajili na utoaji vyeti vya kuzaliwa ili kusitokee matatizo ya aina yeyote.
Dk Migiro amesema mafunzo maalumu juu ya kubaini wanafunzi ambao hawakuzaliwa hapa nchini ili wasiweze kupatiwa vyeti kinyume cha sharia jambo ambalo baadaye linaweza kusababisha maumivu makubwa kwa taifa.
Amesema sheria ya nchi kwa mtoto ipo wazi kwamba mtoto yeyote anayezaliwa hapa nchini ni lazima apatiwe cheti cha kuzaliwa bila kubagua kuwa wazazi wake ni wa taifa gani, ila aliyezaliwa nje ya nchi alafu cheti anataka akipate hapa nchini hiyo ni tofauti
 “Kwa mujibu wa sheria mtoto anapaswa kusajiliwa ili kupatiwa cheti  ndani ya siku 90 baada ya kuzaliwa, kwani Serikali inapanga mipango yake ya maendeleo kutokana na idadi ya watu na mahitaji yao kwa ujumla,” amesema Dk Migiro.
Naye Ofisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Philip Saliboko amesema RITA inatarajia kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa wanafunzi 155,944 katika Manispaa ya kinondoni huku zoezi hilo likizihusisha shule za msingi 140.
Saliboko alisema vyeti vitakavyotolewa kwenye shule hizo kupitia mkakati huu havina tofauti na vinavyotolewa katika ofisi zao na taratibu zote zitafanyika kwa mujibu wa sheria.
“Kuwa na cheti cha kuzaliwa ni nyaraka ya msingi ambayo kila mwananchi anayestahili anapaswa kuwa nayo kwani hutoa uthibitisho wa mahali mtu alipozaliwani taarifa muhimu sana kabla ya kuweza kupata huduma mbalimbali za msingi kwa binadamu,” amesema Saliboko. 
Ameongeza kuwa mkakati huo umeshaanza kutekeleza katika manispaa ya Ilala kwa kuzishirikisha shule 105 na mpaka sasa kuna zaidi ya wanafunzi 16,000 waliosajiliwa na kupatiwa vyeti vya kuzaliwa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment