MCT: MTAALA MPYA VYUO VYA UANDISHI WA HABARI KUBORESHA TAALUMA.

 


BARAZA la Habari Tanzania ( MCT) kwa kushirikiana na  Baraza  la Elimu ya Ufundi (NACTE), hayatakubali kuona viwango cha ufundishaji wa  Vyuo vya Uandishi wa Habari nchini katika  kutumia mtaala mpya ya  taifa yenye ithibati ya Nacte unakwamishwa.
Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania, Kajubi Mukajanga, alibainisha hayo juzi mjini hapa wakati akifungua mafunzo ya matumizi ya mtaala mpya kwa baadhi ya Walimu wa Vyuo zaidi ya tisa  vya Uandishi wa Habari nchini , mafunzo yaliyopangwa kumalizika jana (sept 27), mkoani hapa.
Kwa mujibu wa Katibu Mtendaji wa MCT, mtaala huo  utatumiwa kufundishia wanafunzi wa uandishi wa habari ngazi ya cheti na diploma yaani ngazi za kiufundi za nne , tano na sita ambapo lengo ni kuweka ubora wa taaluma hiyo katika vyuo vya Uandishi wa habari nchini.
“ Vyuo vya Uandishi wa Habari Tanzania vinakatiwa vifikiee katika ngazi ya juu ya ubora kwa cheti na diploma ...kada hii ndio waaandishi wazuri wa habari , hivyo ni muhimu sana kujenga ubora huo kwa kuwa na mtaala mmoja wa kitaifa” alisema Mukajanga
Alisema , mtaala huo ni wa Vyuo vya Uandishi wa Habari na kwamba NACTE pamoja na MCT watasaidia kuboresha na kuhakikisha unatumiwa kufundishia kwenye Vyuo hivyo.
Hata hivyo alisema,  haitoshi kujua kuandika ‘intro’ na baadaye ukajiita  ni mwalimu , bali mwalimu ni zaidi ya kujua kitu cha ziada  kwa ajili ya kuwafundisha wanafunzi.
 Kwa mujibu wa Katibu Mtendaji huo mapema mwakani , NACTE na Baraza hilo watafanya mapitio ya mtaala huo ili kuangalia mapugufu kwa lengo la kufanya maboresho zaidi.
Pia alisema ,  MCT itapo katika mchakato kukutana  na wamiliki wa Vyombo vya Habari nchini ili kupata maoni yao yatakayoweza  kufanikisha kuboresha sekta ya Habari nchini.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment