WAFANYABIASHARA MOROGORO WAANDAMANA KUPINGA MASHINE ZA TRA!!

 

 Wafanya biashara wa Mkoa wa Morogoro wakiwa wamekusanyika wakijadili jambo.
Wafanyabiashara wa Mkoa wa Morogoro wamegoma kufungua maduka leo wakitaka kuonana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa Lengo la kushinikiza kukataa mashine za kieletroniki za mamlaka ya mapato tanzania.Wafanya biashara hao wamegoma kufungua maduka tangu asubuhi wakishinikiza kuonana na mkuu wa mkoa jambo ambalo Mkuu wa mkoa amekubali na kuwaomba wateuliwe wawakilishi 8 kwa ajili ya kwenda kuonana nao.Baada ya wawakilishi kuteuliwa bado wafanyabiashara hao walishinikiza kuandamana mpaka nje ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa ndipo Jeshi la Polisi walipoingilia kati .

Jeshi la Polisi wakiwa barabara inayoelekea Kwenye ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Kulinda Amani na kuzuia maandamano yaliofanywa na wafanyabiashara hao muda huu.

Waduka yakiwa yamefungwa katikati ya Mji wa Morogoro  
 Wafanyabishara hao wakiandamana kuelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro kwa lengo la kushinikiza kuondolewa kwa mashine za Kieletroniki kwa madai kwamba ni kikwazo kikubwa katika biashara zao za kila siku
 


POSTED BY:www.info@dirayetu.blogspot.com


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment