WAYNE ROONEY KUPIGANIA UBINGWA WA 21 MAN UNITED!!

ROONEY-HEADBANDSTAA wa Manchester United Wayne Rooney ameapa kuongeza bidii kuirudisha Timu yake kwenye mbio za Ubingwa huku Klabu hiyo ikiripotiwa kuanza mazungumzo na Mawakala wa Javier Hernandez ‘Chicharito’ ili kuongeza na kuuboresha Mkataba wake.

Hivi karibuni, baada kuanza kwa kusuasua kwenye Ligi Kuu England, Wayne Rooney alikuwa mmoja wa wapiganaji walioirudisha kwenye reli Man United na kuiwezesha kuwafunga Vinara wa Ligi Arsenal Bao 1-0 Jumapili iliyopita na kuwafanya wawe Pointi 5 tu nyuma ya Vinara hao.
Rooney amesema yuko na uchu wa kuipatia Man United Taji la 21 la Ubingwa kwa kuanzia na Pointi 3 Jumapili watakapocheza Ugenini na Cardiff City.
Rooney, mwenye Miaka 28, amesema: “Siku zote nimesema Kombe muhimu kwenye Msimu wowote ni Ligi Kuu. Ndio Ligi yenu ya Nyumbani na hiyo huamua nani bora kwa Msimu wote. Hiyo ndio muhimu kushinda!”
WAKATI HUO HUO, Manchester United inajiandaa kufungua mazungumzo ili kumpa MkatabaCHICHARITO_SHANGILIAmpya Straika wao Javier Hernandez ‘Chicharito’ na kumthibitishia kwamba bado anahitajika hapo Old Trafford.
Hivi sasa, kwa kupewa namba, Chicharito yupo nyuma ya Robin van Persie na Wayne Rooney ambapo pia inabidi apigane na Danny Welbeck ili kupata nafasi.
ANDERS_LINDEGAARDJambo hilo limezua minong’ono kuwa Straika huyo kutoka Mexico anataka kuhama huku Arsenal na Tottenham pamoja na Timu ya Spain, Atletico Madrid, zikitajwa.
Lakini Bosi wa Man United, David Moyes, ameshatoa bayana kuwa Chicharito, mwenye Miaka 25 yupo kwenye mipango yake.
Hivi sasa inasemekana Chicharito, ambae Mkataba wake umebakisha Miaka miwili, atapewa Mkataba mpya ambao utaboreshwa na huenda akalipwa maradufu ya Pauni 60,000 kwa Wiki anazolipwa sasa.
Mchezaji ambae huenda akang’oka Man United ni Kipa Anders Lindegaard kutoka Denmark ambae ameshindwa kumng’oa David de Gea kama Kipa Nambari Wani.
Ipo minong’ono kuwa Lindegaard huenda akaenda Italy.
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumamosi 23 Novemba
1545 Everton v Liverpool
1800 Arsenal v Southampton
1800 Fulham v Swansea City
1800 Hull City v Crystal Palace
1800 Newcastle United v Norwich City
1800 Stoke City v Sunderland
2030 West Ham United v Chelsea
Jumapili 24 Novemba
1630 Manchester City v Tottenham Hotspur
1900 Cardiff City v Manchester United
Jumatatu 25 Novemba
2300 West Bromwich Albion v Aston Villa
MSIMAMO WA LIGI KUU ENGLAND

NA
TIMU
P
GD
PTS
1
Arsenal
11
12
25
2
Liverpool
11
11
23
3
Southampton
11
10
22
4
Chelsea
11
8
21
5
Man Utd
11
5
20
6
Everton
11
4
20
7
Tottenham
11
3
20
8
Man City
11
16
19
9
Newcastle
11
-1
17
10
West Brom
11
0
14
11
Aston Villa
11
-1
14
12
Hull
11
-5
14
13
Swansea
11
0
12
14
Cardiff
11
-6
12
15
Norwich
11
-12
11
16
West Ham
11
-2
10
17
Stoke
11
-4
10
18
Fulham
11
-9
10
19
Sunderland
11
-14
7
20
Crystal Palace
11
-15
4

POSTED BY:www.info@dirayetu.blogspot.com

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment