 STAA
 wa Manchester United Wayne Rooney ameapa kuongeza bidii kuirudisha Timu
 yake kwenye mbio za Ubingwa huku Klabu hiyo ikiripotiwa kuanza 
mazungumzo na Mawakala wa Javier Hernandez ‘Chicharito’ ili kuongeza na 
kuuboresha Mkataba wake.
STAA
 wa Manchester United Wayne Rooney ameapa kuongeza bidii kuirudisha Timu
 yake kwenye mbio za Ubingwa huku Klabu hiyo ikiripotiwa kuanza 
mazungumzo na Mawakala wa Javier Hernandez ‘Chicharito’ ili kuongeza na 
kuuboresha Mkataba wake.
Hivi karibuni, baada kuanza kwa kusuasua
 kwenye Ligi Kuu England, Wayne Rooney alikuwa mmoja wa wapiganaji 
walioirudisha kwenye reli Man United na kuiwezesha kuwafunga Vinara wa 
Ligi Arsenal Bao 1-0 Jumapili iliyopita na kuwafanya wawe Pointi 5 tu 
nyuma ya Vinara hao.
Rooney amesema yuko na uchu wa kuipatia 
Man United Taji la 21 la Ubingwa kwa kuanzia na Pointi 3 Jumapili 
watakapocheza Ugenini na Cardiff City.
Rooney, mwenye Miaka 28, amesema: “Siku 
zote nimesema Kombe muhimu kwenye Msimu wowote ni Ligi Kuu. Ndio Ligi 
yenu ya Nyumbani na hiyo huamua nani bora kwa Msimu wote. Hiyo ndio 
muhimu kushinda!”
WAKATI HUO HUO, Manchester United inajiandaa kufungua mazungumzo ili kumpa Mkataba mpya Straika wao Javier Hernandez ‘Chicharito’ na kumthibitishia kwamba bado anahitajika hapo Old Trafford.
mpya Straika wao Javier Hernandez ‘Chicharito’ na kumthibitishia kwamba bado anahitajika hapo Old Trafford.
 mpya Straika wao Javier Hernandez ‘Chicharito’ na kumthibitishia kwamba bado anahitajika hapo Old Trafford.
mpya Straika wao Javier Hernandez ‘Chicharito’ na kumthibitishia kwamba bado anahitajika hapo Old Trafford.
Hivi sasa, kwa kupewa namba, Chicharito 
yupo nyuma ya Robin van Persie na Wayne Rooney ambapo pia inabidi 
apigane na Danny Welbeck ili kupata nafasi.
 Jambo
 hilo limezua minong’ono kuwa Straika huyo kutoka Mexico anataka kuhama 
huku Arsenal na Tottenham pamoja na Timu ya Spain, Atletico Madrid, 
zikitajwa.
Jambo
 hilo limezua minong’ono kuwa Straika huyo kutoka Mexico anataka kuhama 
huku Arsenal na Tottenham pamoja na Timu ya Spain, Atletico Madrid, 
zikitajwa.
Lakini Bosi wa Man United, David Moyes, ameshatoa bayana kuwa Chicharito, mwenye Miaka 25 yupo kwenye mipango yake.
Hivi sasa inasemekana Chicharito, ambae 
Mkataba wake umebakisha Miaka miwili, atapewa Mkataba mpya ambao 
utaboreshwa na huenda akalipwa maradufu ya Pauni 60,000 kwa Wiki 
anazolipwa sasa.
Mchezaji ambae huenda akang’oka Man 
United ni Kipa Anders Lindegaard kutoka Denmark ambae ameshindwa 
kumng’oa David de Gea kama Kipa Nambari Wani.
Ipo minong’ono kuwa Lindegaard huenda akaenda Italy.
LIGI KUU ENGLAND
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumamosi 23 Novemba
1545 Everton v Liverpool
1800 Arsenal v Southampton
1800 Fulham v Swansea City
1800 Hull City v Crystal Palace
1800 Newcastle United v Norwich City
1800 Stoke City v Sunderland
2030 West Ham United v Chelsea
Jumapili 24 Novemba
1630 Manchester City v Tottenham Hotspur
1900 Cardiff City v Manchester United
Jumatatu 25 Novemba
2300 West Bromwich Albion v Aston Villa
MSIMAMO WA LIGI KUU ENGLAND
| NA | TIMU | P | GD | PTS | 
| 1 | Arsenal | 11 | 12 | 25 | 
| 2 | Liverpool | 11 | 11 | 23 | 
| 3 | Southampton | 11 | 10 | 22 | 
| 4 | Chelsea | 11 | 8 | 21 | 
| 5 | Man Utd | 11 | 5 | 20 | 
| 6 | Everton | 11 | 4 | 20 | 
| 7 | Tottenham | 11 | 3 | 20 | 
| 8 | Man City | 11 | 16 | 19 | 
| 9 | Newcastle | 11 | -1 | 17 | 
| 10 | West Brom | 11 | 0 | 14 | 
| 11 | Aston Villa | 11 | -1 | 14 | 
| 12 | Hull | 11 | -5 | 14 | 
| 13 | Swansea | 11 | 0 | 12 | 
| 14 | Cardiff | 11 | -6 | 12 | 
| 15 | Norwich | 11 | -12 | 11 | 
| 16 | West Ham | 11 | -2 | 10 | 
| 17 | Stoke | 11 | -4 | 10 | 
| 18 | Fulham | 11 | -9 | 10 | 
| 19 | Sunderland | 11 | -14 | 7 | 
| 20 | Crystal Palace | 11 | -15 | 4 | 
0 comments:
Post a Comment