Mwezeshaji wa warsha hiyo ambaye pia ni Mkufunzi wa Redio za Jamii kutoka Unesco, Mama Rose Haji Mwalimu, akitoa
 utambulisho kwa waendesha warsha ya namna ya kuandika habari za 
migogoro kutoka Shirika la Search for Common Grounds (SFCG), 
yanayoendelea mjini Dodoma.
Meneja
 Mradi wa SFCG wilaya ya Tarime, Bwana Jacob Mulikuza, akielezea maudhui
 ya warsha ya namna ya kuandika habari za migogoro kwa washiriki ambao 
ni waandishi wa redio za jamii kutoka Tanzania, warsha hiyo inafanyika 
mjini Dodoma.
Washiriki
 wa warsha wakimsikiliza Bw. Jacob Mulikuza kutoka Shirika la Search for
 Common Grounds – SFCG (hayupo pichani) akielezea jambo wakati wa warsha
 ya namna ya kuandika habari za migogoro inayoendelea mjini Dodoma kwa 
waandishi na watangazaji wa Redio za Jamii nchini iliyofadhiliwa na 
UNESCO kupitia mradi wa DEP.
Mmoja
 wa washiriki akifafanua jambo katika warsha hiyo iliyojadili namna ya 
kuandika habari za migogoro kutoka Shirika la Search for Common Grounds 
(SFCG) yanayoendelea mjini Dodoma.
Meneja
 mradi wa SFCG wilaya ya Tarime, Bwana Jacob Mulikuza, akiwapatia 
maelekezo washiriki wa warsha ya namna ya kuandika habari za migogoro 
kuhusu namna ya uwajibikaji katika kutatua migogoro ndani ya Jamii.
Mmoja
 wa washiriki Bwana Baraka kutoka ORS Fm Radio, akiwaelezea washiriki 
wenzaka namna Ya kutatua fumbo lililokuwa sehemu ya kazi za Vikundi, 
katika warsha ya Uandishi wa habari za Migogoro kuhusu namna ya 
uwajibikaji katika kutatua migogoro ndani ya Jamii.
Mratibu
 wa vyombo vya habari wa SFCG Zanzibar, Bwana Ali sultan, akielezea 
kuhusu ushiriki wa SFCG huko Zanzibar katika warsha ya namna ya kuandika
 habari za migogoro kwa washiriki ambao ni waandishi wa Redio za Jamii 
kutoka Tanzania, warsha hiyo inayofanyika mjini Dodoma imefadhiliwa na 
Shirika la UNESCO kupitia mradi wa Demokrasia na Amani (DEP) kuelekea 
Uchaguzi 2015.
Meneja
 Mawasiliano wa SFCG kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bwana 
Dupont Ntererwa, akielezea kuhusu ushiriki wa SFCG huko DRC katika 
warsha ya namna ya kuandika habari za migogoro kwa washiriki ambao ni 
Waandishi wa Redio za Jamii kutoka Tanzania, warsha hiyo inayofanyika 
mjini Dodoma









0 comments:
Post a Comment