Upigaji kura waanza Nchini Thailand Leo!!

Raia wa Thailand wanapiga kura leo Jumapili(02.02.2014)chini ya ulinzi mkali katika uchaguzi ambao unaweza kuitumbukiza nchi hiyo iliyogawika katika mzozo mkubwa zaidi wa kisiasa.

Thailand Wahlen Wahllokale Zoezi la upigaji kura limeanza
Mzozo huo wa kisiasa utasababisha mshindi kushindwa kufanyakazi kwa miezi kadhaa kutokana na maandamano ya mitaani, kesi mahakamani na mivutano bungeni.
Zoezi la upigaji kura lilianza kwa amani siku moja baada ya watu saba kujeruhiwa kwa kupigwa risasi na miripuko wakati wa mapambano kati ya waungaji mkono na wapinzani wa waziri mkuu Yingluck Shinawatra katika eneo la kaskazini la mji mkuu Bangkok ambalo ni ngome kuu ya chama chake cha Puea Thai.

Thailand Bangkok Proteste Wahl Anti Regierung 1.2.14 Waandamanaji wakionesha upinzani wao dhidi ya upigaji kura
Upigaji kura ulisitishwa katika wilaya na baadhi ya vituo vingine vya upigaji kura vilishindwa kufunguliwa kwasababu ya mbinyo kutoka kwa waandamanaji wanaoipinga serikali. Upigaji kura nje ya mji mkuu na upande wa kusini haukuathirika.
"Hali kwa jumla ni shwari na hatujapokea ripoti zozote za ghasia asubuhi ya leo," mkuu wa baraza la usalama la taifa Paradorn Pattanatabutr ameliambia shirika la habari la Reuters. "Waandamanaji wanafanya maandamano kwa amani kuonesha upinzani wao dhidi ya uchaguzi huo."
Wapiga kura wana hofu
Mabango ya kawaida kwa ajili ya kampeni , na picha kubwa na hali ya shauku ya uchaguzi havionekani , pamoja na mamilioni ya wapiga kura ambao wanahofu ya kutokea ghasia ama wanaelemea kupinga zoezi hilo la uchaguzi lenye lengo la kuurejesha tena madarakani uongozi wa kisiasa unaodhibitiwa na kaka yake waziri mkuu Yingluck ambaye ni tajiri mkubwa, Thaksin Shinawatra.
Demonstrationen in Bangkok Waandanamaji wakipinga zoezi la kupiga kura
Thaksin, mwenye umri wa miaka 64, anapendwa na kuogopewa nchini Thailand, lakini vyama vyake vimeshinda kila uchaguzi tangu mwaka 2001. Wapinzani wake wanasema kuwa ni bepari mpenda rushwa ambaye anatawala kwa kumtumia dada yake wakati yeye binafsi akiwa uhamishoni nchini Dubai.
Kuna haja ya mabadiliko
"Hatuzuwii uchaguzi. Tunauahirisha tu," amesema Nipon Kaewsook, mwenye umri wa miaka 42, mmoja katika ya mamia ya waandamanaji wanaozuwia ofisi ya wilaya ya Ratchathewi katikati ya mji mkuu Bangkok wakizuwia usambazaji wa makasha ya karatasi za kupigia kura.
"Bado tunahitaji uchaguzi, lakini tunahitaji kwanza mabadiliko ," ameongeza Nipon, mwalimu wa lugha ya kiingereza kutoka Phattalung kusini mwa Thailand.
Waandamanaji waliimba "Yingluck achia ngazi" na "Thaksin afungwe"! Wameondoa picha zilizokuwa zimewekwa mbele ya masanduku ya kura na kuzipeleka katika eneo la kuegesha magari nyuma ya jengo.
Sherehe za ushindi za Yingluck huenda zikawa za chini chini tu.
Thailand Bangkok Proteste Wahl Anti Regierung 1.2.14 Waandamanaji katika mitaa ya mjini Bangkok
Katika wakati ambapo viti bungeni havitaweza kukamilika, anaweza kujikuta katika hali ngumu, akikabiliwa na kesi mahakamani na kutoshindwa kupitisha miswada na bajeti muhimu ya kufufua uchumi ambao unayumba.
CHANZO: DW
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment