WALIOPATWA NA MAAFA YA MVUA NA UPEPO HAI WATEGEMEA KUNUFAIKA NA MISAADA ZAIDI!!

Na Emanueli Ndanshau

HAI
Baada ya maafa ya Mvua kubwa na upepo mkali iliyosababisha maafa katika maeneo mengi ya wilaya ya Hai,hali hiyo imeanza kutumika ndivyo sivyo na baadhi ya wananchi wakitegemea kunufaika na misaada zaidi.

Hali hiyo imekuwa ikitumiwa na mwanamama anayefahamika kwa jina la Aziza Mohammed ambaye kutokana na taharuki ya upepo na mvua hiyo alilazimika kukimbilia katika choo chake cha kisasa ambacho alijenga kikiwa imara kuliko nyumba yake ya kuishi siku chache kabla ya tukio.



Bibi Aziza Mohammed akiwa katika pozi la kawaida mara anaposikia makundi mbalimbali yanatembelea eneo la maafa pamoja na mjukuu wake ambaye ana matatizo ya akili
Baada ya tufani hilo kutulia na makundi mbalimbali ya watu wakiwemo viongozi kuanza kutembelea maeneo hayo ndipo alipobaini kuwa kukaa kwake chooni kunaweza kumpatia misaada na kuamua kufanya hivyo kwa kila anapopewa taarifa ya ujio wa viongozi katika eneo hilo.

Tofauti na wenzake waliopata maafa ambao waliombewa makazi ama kukaribishwa kwa majirani,lakini  kwa Bibi Aziza ilikuwa ni patashika kukubali kuhama mpaka pale viongozi wa Kata na Kijiji pamoja na maofisa wa Maendeleo ya Jamii walipoenda kumshawishi na kukubali kuhama.

Hata hivyo hakuweza kuridhika hadi baada ya kubaini kuwa atapatiwa msaada wa bati za kutosheleza vyumba viwili ambavyo vitajengwa kwa kununuliwa tofali za kuchoma na wasamaria wema na hivyo kukubali kurudishwa na baadhi ya waandishi wa habari ili kwenda kupigwa picha kule chooni akichukuliwa kutoka kule alikopewa hifadhi.

Hatua hiyo ilijitokeza baada ya kutoridhika na vyumba viwili na kuwaeleza waandishi wa habari hao kuwa mkoa na wilaya umeshindwa kumsaidia na hivyo anamsubiri Waziri mkuu Mizengo Pinda

"Ni kweli ilikuwa ni patashika kumwamisha huyo mama kutokana na mtazamo wake kwamba akiishi hapo chooni baada ya nyumba yake kuezuliwa paa atapata misaada,lakini viongozi wa kitongoji,kijiji na wa maendeleo ya jamii walimwelimisha baadaye alikubali,lakini cha ajabu,leo waandishi wa habari hao wamemchukuwa na kumrudisha kule chooni ili kupata picha" alisema mmoja wa viongozi wa kitongoji

Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga ameeleza kuwa serikali wilayani humo kwa kushirikiana na mbunge wa jimbo la Hai,Freeman Mbowe wameweka mazingira ya dharura ya kusaidia kaya ambazo makazi yao yapo katika hali mbaya yakiwemo ya Bibi Aziza na wengine wengi kwa kutenga fedha za kununua matofali ya kuchoma.


Mkuu wa wilaya ya Hai,Novatus Makunga[Kulia] akipokea msaada wa mabati kutoka kwa viongozi wa kiwanda cha Bonite Bottlers cha mjini Moshi na tofali imara za kuchoma za vyumba viwili hazipo pichani
Makunga ameeleza kuwa pamoja na kuwepo kwa msaada wa mabati 200 kutoka kwa Mwenyekiti wa makampuni ya IPP kupitia Bonite Bottlers,lakini ni vigumu kuezeka katika nyumba nyingi kutokana na kukosa uimara ikiwemo aliyekuwa akiishi Bibi Aziza na hivyo wanajipanga kumnunulia

Lakini pia alisema kuwa msaada kama huo utapelekwa kwa mzee aliyemtaja kwa jina moja la mzee Omar wa kitongoji cha kijiweni ambaye hana msaada kabisa pamoja na mama mjane wa kijiji cha Kikavu Chini ambaye atapatiwa bati lakini kijiji kimekubali kufanya harambe ya kumsaidia kukamilisha nyumba yake.


Makunga ameeleza kutokana na uchache wa msaada hasa bati bado uchanganuzi unafanyika ili kuweza kuzigawa kwa wale ambao wana hali mbaya zaidi.


Aidha Makunga amefafanua kwamba serikali wilayani humo haijawahi kuwaleta waandishi wa habari kupiga picha jinsi wananchi wanavyoishi bali kama ilivyo kwa majukumu ya waandishi wa habari kufanyakazi bila ya mipaka wamekuwa wakija na wasamaria wema wanaoleta misaada kwa lengo la kutaka kujua hali ya maafa hayo.

 Nae Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Mhe Leonidas Gama,ni alikuwa miongoni mwa viongozi waliotembelea vijiji vitano vya ukanda wa tambarare vilivyokumbwa na maafa ya mvua na upepo mkali katika wilaya ya Hai kwa lengo la kuwafariji waliokumbwa na maafa hayo.
Mhe Gama aliwafariji wananchi wa vijiji hivyo vya Shirimgungani,Mijongweni,Kwatito,Ngosero na Kikavu Chini.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh Leonidas Gama akizungumza na wathirika wa maafa Hai
Mkuu huyo wa mkoa aliwahakikishia wananchi hao kuwa serikali ipo pamoja nao katika kuhakikisha kuwa wanajikimu kimaisha kwa kuwa na mahitaji ya msingi ya chakula ambacho kitawapa nguvu ya kujipanga upya kwa maisha.

 Aliuagiza uongozi wa wilaya kuangalia uwezekano wa kuwa na mbegu fupi za mahindi zinazokomaa kwa muda mfupi ili wananchi hao ambao hivi sasa wanajiandaa kwa msimu wa kilimo wawe na uhakika wa kupata mavuno ya kutosha.

Alisema kutokana na mazingira yanayojitokeza ya mvua za sasa kuja kwa kasi lolote linaweza kutokea likiwemo la mvua hizo kukata kwa muda mfupi.

Aidha Mheshimiwa Gama aliutaka uongozi wa wilaya sasa kuwa na programu ya kuhakikisha wananchi wanakuwa na nyumba imara ili kuepukana na maafa ya kila mwaka pale zinapojitokeza mvua kubwa zinazoambanatana na upepo
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment