LIGI KUU ENGLAND: ROONEY KUIKOSA NEWCASTLE LEO!!


ROONEY_N_RVPSTRAIKA hatari wa Manchester United, Wayne Rooney, Leo Jioni hatacheza Mechi ya Ligi Kuu England dhidi ya Newcastle huko Saint James Park kwa sababu ya kuumia kidole gumba cha Mguuni.

Maumivu hayo pia yameleta wasiwasi mkubwa kama atakuwa fiti kwa ajili ya Mechi ya Marudiano ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL, hapo Jumatano huko Allianz Arena, Jijini Munich watakapoivaa tena Bayern Munich baada kutoka 1-1 Jumanne iliyopita huko Old Trafford.

Rooney, mwenye Miaka 28, aliumia kwenye Mechi hiyo na Bayern Munich lakini alimaliza Dakika zote 90.
Rooney sasa anaungana kwenye Safu ya Majeruhi pamoja na Straika mwingine mkubwa, Robin van Persie, ambae aliumia Goti Mwezi uliopita walipoitandika Olympiakos Bao 3-0 kwenye UCL na kufuzu kucheza na Bayern Munich huku Van Persie akifunga Bao zote hizo 3.

Akiongea na MUTV, Kituo cha TV cha Man United, Meneja wa Man United, David Moyes alisema: "Rooney amechubuka vibaya Kidole Gumba cha Mguu. Ni tatizo kwa Mechi hii na Newcastle lakini pia inaweza kuwa tatizo kwa Mechi huko Munich. Inabidi tumwangalie.”

Kukosekana kwa Rooney na Van Persie kunatoa nafasi kwa Danny Welbeck na Javier Hernandez ‘Chicharito’ kupata nafasi za kucheza.
Kuhusu Robin van Persie, David Moyes amesema anaendelea vizuri na matibabu na yupo njiani kurejea Uwanjani.

Van Persie, ambae alitabiriwa atakuwa nje ya Uwanja hadi Wiki 6, ameshazikosa Mechi dhidi ya West Ham, Manchester City, Aston Villa na Bayern Munich.

Hapo Jana, akiongea na Wanahabari kuhusu Mechi ya Leo na Newcastle, Moyes amesema: "Robin yupo Holland akitibiwa na tunapata Ripoti zake kila Siku, anaendelea vizuri!"
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment