HALIMA MDEE NA WENZAKE KUPANDISHWA KIZIMBANI LEO!!





 










 




Mbunge wa jimbo la Kawe kwa tiketi ya Chadema, Halima Mdee (35) pamoja na wenzake wanane wanaokabiliwa na mashtaka yakutotii amri ya Jeshi la polisi wanatarajia kusomewa maelezo ya awali leo katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.

Mdee ambaye pia ni mwenyekiti wa Baraza la wanawake Chadema {BAWACHA} pamoja na wanachama wenzake watasomewa maelezo hayo mbele ya hakimu mkazi Janeth Kaluyenda, kwakuwa upelelezi wa kesi hiyo umeshakamilika.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Rozi Moshi (45) mkazi wa Kinondoni B,renina Peter alimaarufu kama Lufyagila mkazi wa Kinondoni Mkwajuni,Anna Linjewile (48) mkazi wa Mbezi Luisi na Mwanne Kassim (32) Mkazi  wa Pugu Kajiungeni.

Wengine ni Sophia Fangel (28) mkazi wa Mbezi Beach, Edward Julius (25) mkazi wa Msasani, Martha Mtiko (27) mkazi wa Mikocheni A, pamoja na Beatu Mmari (35) mkazi wa Kinondoni Mkwajuni. 

Aidha washtakiwa hao wanadaiwa kuwa mnamo octoba 4 mwaka huu katika mtaa wa Ufipa bila ya kuwa na uhalali walikiuka amri halali yakutawanyika iliyotolewa na Mrakibu wa Polisi (SP) Emmanuel Tillf kwaniaba ya jeshi la Polisi.

Vilevile washtakiwa hao inadaiwa siku hiyo katika eneo hilo kwa pamoja walifanya mkusanyiko usio halali kwa lengo lakutembea kwenda Ofisi ya Rais.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment