KAMATI KUU YA CHADEMA KUKUTANA KUJADILI MAFANIKIO YA UKAWA!!

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),itafanya mkutano maalumu kwa ajili ya kupokea taarifa na kujadili mambo mbalimbali, ikiwemo ushirikiano mzuri ulioneshwa na Umoja wa Katiba ya Wananchi(UKAWA)katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa CHADEMA, Tumaini Makene, alisema mada mbalimbali zitajadiliwa na kamati hiyo itatoa maamuzi ya nini kifanyike.

Alisema pia kikao hicho kitapokea taarifa ya ushirikiano wa UKAWA jinsi unavyoendelea, kwani ushirikiano huo umeonesha matumaini makubwa kwao kutokana na kuonesha matunda mazuri katika chaguzi za serikali za mitaa.

Alisema kamati hiyo inafanya kikao maalumu kwa ajili ya kupokea taarifa na kujadili mambo mbalimbali kuhusu sintofahamu kuhusiana na uandikishaji wa Daftari la Wapigakura kwa kutumia mfumo wa BBR.

Hata hivyo, alisema katika maeneo ambayo mfumo huo umeanza kwa majaribio umeonesha udhaifu mkubwa wa hali ya juu; hivyo umefeli kwa kiasi kikubwa.

Pia alitaja mada nyingine zitakazojadiliwa kuwa ni pamoja na maandalizi ya upigaji kura ya maoni kutokana na muda mfupi uliobaki kuwa mdogo.

Alisema elimu kwa wananchi inatakiwa kutolewa miezi miwili na kuwepo muda wa kufanya kampeni. Vile vile alisema watapokea taarifa mbalimbali kutoka kwa wataalamu wa chama hicho, wanasheria pamoja na sekretarieti kuu ya chama na pia itajadili kuelekea Uchaguzi Mkuu wa urais, wabunge na madiwani.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment