KATIBU MKUU WA CCM ASEMA ITAKUWA NDOTO UPINZANI KUSHIKA DOLA!!

 katibu mkuu wa chama cha mapinduzi ccm <b>abdulrahman kinana</b> amesema ...

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. Abdulrahman Kinana, amesema ni jambo lisilowezekana kwa Chama cha Wananchi (CUF), kushika dola kama wanavyoamini viongozi na wanachama wao bali jambo hilo haliwezekani duniani labda mbinguni.

Bw. Kinana aliyasema hayo juzi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Magereza, Kata ya Tomondo, Wilaya ya Dimani, Mkoa wa Magharibi, Zanzibar.

Alisema pamoja na CUF kuunda Serikali ya Kitaifa Zanzibar, bado imeshindwa kuwasaidia wananchi badala yake viongozi wa chama hicho wanaendekeza safari za nje ya nchi.

"Wana CUF msikubali kudanganywa na hotuba nzuri za viongozi wenu, mtasikia hiki na kile lakini mwisho wa siku hamna kitu, viongozi wenu wamepewa Wizara mbalimbali tena muhimu lakini mbona hawatoi ajira wakidai kusubiri urais, hilo haliwezekani hadi kiama.

"Mimi nadhani, Mawaziri wa CUF walipaswa kutumia fursa hizo kujiimarisha kwa kuwatumikia wananchi, kuwajengea shule, zahanati na kutoa ajira badala yake, viongozi wenu kila siku wapo nje ya nchi hasa Uarabuni kwa masilahi yao, wangeweza kutumia nafasi hiyo lakini wanataka urais," alisema Bw. Kinana.

Aliwataka wana CCM kuteua wagombea wanaokubalika kwenye jamii badala ya kuwapitisha wagombea wenye nguvu za fedha kwani wakishindwa wanaunda magenge ya kukisaliti chama.

Alisema lazima wana CCM wakubali matokeo wanaposhindwa katika nafasi mbalimbali wanazogombea ili kukinusuru chama kwani wapo baadhi ya wanachama ambao wakishindwa wanakwenda kujiunga na upinzani.

"Chagueni wagombea wanaokubalika katika jamii ambao watakuwa waadilifu, wanaowajali wananchi na wachapa kazi, msiwachague wanaogawa fedha ambao wakishindwa wanasema heri tukose wote, mchana wanajifanya CCM, usiku CUF," alisema.

Alisema CCM kimejiimarisha kuendelea kushika dola kikitekeleza ilani zake kwa vitendo tofauti na wapinzani ambao kazi yao ni kutoa ahadi hewa kwa wananchi wanapoomba kura.

Chanzo:majira

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment