LIGI KUU ENGLAND: JUMANNE & JUMATANO TIMU ZOTE 20 UWANJANI!!

 
BAADA ya Mechi za Wikiendi, Timu zote 20 za Ligi Kuu England zitajitupa tena Uwanjani Jumanne na Jumatano Usiku kucheza Mechi zao za raundi ya 25 za Msimu huu.
 
Siku ya Jumanne Usiku zipo Mechi 4 na Siku ya Jumatano zipo Mechi 6.Katika mechi hizo
kwa siku ya Jumanne, Arsenal, ambao wapo Nafasi ya 6, wapo kwanye uwanja wao wa nyumbani Emirates kucheza na Leicester City ambayo iko mkiani ikishikilia  Nafasi ya 20.

Mechi nyingine kali ya siku hiyo ya Jumanne ni ile ya kule Anfield wakati Liverpool, walio Nafasi ya 7, watakapo ikaribisha Tottenham ambayo iko Nafasi ya 5 ikiwa Pointi 4 mbele ya Liverpool.
Mechi za Jumatano Usiku ni pamoja na ile ya Vinara wa Ligi, Chelsea, watakaokuwa kwao Stamford Bridge kucheza na Everton wakati kule Old Trafford, Manchester United, ambayo ipo Nafasi ya 4, itawakaribisha Burnley walio Nafasi ya 17.
Mabingwa Watetezi wa Ligi, Man City, wao watakuwa Wageni huko Britannia Stadium kucheza na Timu ngumu Stoke City.
Timu iliyo Nafasi ya 3, Southampton, wao wapo Nyumbani kwao Saint Mary’s kuivaa Timu kali Msimu huu, West Ham United.

RATIBA:
**Saa za Bongo
Jumanne Februari 10
2245 Arsenal v Leicester            
2245 Hull v Aston Villa               
2245 Sunderland v QPR             
2300 Liverpool v Tottenham                
Jumatano Februari 11
2245 Chelsea v Everton             
2245 Man United v Burnley                  
2245 Southampton v West Ham           
2245 Stoke v Man City               
2300 Crystal Palace v Newcastle           
2300 West Brom v Swansea  
      
MSIMAMO:
TEBO-BPL-FEB8
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment