TAKUKURU YAMNASA HAKIMU KWAKUOMBA NA KUPOKEA RUSHWA KILIMANJARO!!


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imemnasa Hakimu mmoja wilayani Mwanga, mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma za kuomba na kupokea rushwa ya Sh500,000.
 
Tukio hilo lililovuta hisia za wananchi wengi wa wilaya hiyo na wadau wa tasnia ya sheria, lilitokea jana saa 10:00 jioni katika baa moja iliyopo jirani na mahakama ya wilaya hiyo.
Habari za uhakika zilizopatikana leo na kuthibitishwa na baadhi ya maofisa wa Takukuru, zilisema kabla ya mtego huo, Hakimu huyo alikuwa amepokea Sh500,000 kwa M-Pesa.
Kwa mujibu wa habari hizo, Hakimu huyo aliomba rushwa hiyo ili aweze kutoa dhamana kwa mtuhumiwa mmoja aliyekuwa mahabusu katika gereza la Kiruru la wilayani Mwanga.
Jina la Hakimu huyo ambaye jana alihamishiwa mjini Moshi kwa mahojiano, tunalihifadhi kwa sasa kwa sababu za kimaadili.
 “Kuna bwana yuko gerezani alishindwa kutimiza masharti ya dhamana kwa hiyo mheshimiwa (Hakimu) akamwambia mkewe ampe Sh500,000 ili ampatie dhamana,” kilidokeza chanzo chetu.
Mtoa habari huyo alidai, mke wa mtuhumiwa huyo alimtumia Hakimu huyo Sh500,000 kwa njia ya M-Pesa lakini akashangaa mumewe kutopewa dhamana na Hakimu huyo.
Inadaiwa badala yake, Hakimu huyo alitaka aongezewe Sh500,000 nyingine na ndipo mke wa mtuhumiwa huyo alipotoa taarifa Takukuru na mtego kuandaliwa.
Taarifa za kukamatwa kwa Hakimu huyo zilizagaa kwa kasi kuanzia jana usiku huku wananchi wa kawaida na mahakimu wakitumiana meseji wakihabarishana juu ya tukio hilo.
Jitihada za kumpata Kamanda wa Takukuru mkoa Kilimanjaro, Lawrence Swema ili kuthibitisha au kukanusha tukio hizo, hazikuzaa matunda kwani simu yale ilikuwa ikiita bila majibu na meseji hazijibiwi.
Chanzo: Mwananchi
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment