WAHITIMU MAFUNZO YA JKT MWAKA 2004-2006 WAIOMBA SERIKALI KUWAPATIA AJIRA!!


Vijana zaidi ya 30,000 waliomaliza mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) nchini Tanzania katika miaka ya 2004 – 2006 wameiomba serikali kuangalia namna watakavyoweza kuwapatia ajira kutokana na kukaa muda mrefu bila ya kuwa na ajira.
Wakizungumza kwa niaba ya vijana hao leo jijini Dar es Salaam mara baada ya kukusanyika kwa pamoja viongozi wa vijana hao wamesema wamefanya jitihada mbalimbali za kutaka kukutana Rais Jakaya Kikwete kwa lengo la kumueleza matatizo yao lakini wamekuwa wakikumbana na vikwazo vikiwemo vya kuzuiliwa na jeshi la polisi.
 
Wamesema kwa sasa wanahangaika kutokana na kukosa ajira huku wakiwa na ujuzi wa kutosha kutokana na mafunzo ya kijeshi waliyoyapata hivyo ni vema serikali ikaangalia uwezekano wa kuwapatia ajira vijana hao ili kuepukana na vishawishi vinavyoweza kujitokeza.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment