WAPENDEKEZA NAULI ZA DALADALA ZIPUNGUZWE!!

Daladala zikiwa katika stendi ya Ubungo jijini Dar es Salaam tayari kupakia abiria. Picha na Maktaba 
Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Usafiri wa Nchi Kavu na Majini Sumatra (Sumatra-CCC), wameishauri Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kupunguza nauli za mabasi, ikiwamo daladala kwa asilimia 15 hadi 24.

Ushauri huo umekuja siku tatu tangu Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura), kupunguza bei ya mafuta kwa mara nyingine katika kipindi cha miezi mitatu, huku punguzo la sasa likitajwa kuwa ni la chini zaidi katika kipindi cha miaka sita iliyopita.
Katibu mtendaji wa baraza hilo, Dk Oscar Kikoyo alisema kwa kuwa punguzo hilo limefikia Sh1,652 kwa petrol na Sh1,563 kwa dizeli, huku mafuta ya taa yakiuzwa Sh1,523, kuna haja ya mamlaka hiyo kupunguza nauli za mabasi kwa asilimia 15 hadi 24.
“Katika ukokotoaji, ikiwa wamiliki wa mabasi watapata faida ya asilimia 25 hadi 30, lazima nauli ishuke ili kuendana na mtiririko uliopo ili kuleta mlingano ulio sawa,” alisema Dk Kikoyo na kuongeza:
“Baada ya kuangalia mfumo wa ukokotoaji, tumependekeza kwa Sumatra ishushe nauli kwa mlingano wa asilimia 15-24. Kwa hiyo, nauli za daladala zishuke kwa Sh50, huku mikoani mfano Dar mpaka Arusha ishuke kutoka Sh36,000 mpaka Sh28,000.”
Dk Kikoyo alisema kuwa baraza limekuwa likikusanya takwimu tangu kushuka kwa bei mwishoni mwa mwaka jana na kuendelea na ukokotoaji.
“Tumeangalia mambo mengi kwani licha ya mafuta kushuka bei, vipuri vya magari vipo juu. Lakini tunaamini kushuka nauli kutaleta tija kwa mtumiaji, maana kuna wengine wanashindwa kusafiri kutokana na gharama kuwa juu,” alisema Dk Kikoyo.
Hii ni mara ya pili mafuta kushuka bei hadi kufikia Sh1,652. Awali, iliwahi kutokea Mei mwaka 2009, ambapo bei ya petroli ilishuka kutoka Sh2,200 hadi Sh1,147 na ikapanda tena kwa hadi kufikia Sh2,000 na zaidi. Baada ya hapo haikuwahi kushuka hadi mwishoni mwa mwaka jana iliposhuka kwa Sh1,768.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment