MCHAKATO WA UCHAMBUZI WA RASIMU YA KATIBA WAENDELEA KATIKA CHUO CHA UANDISHI WA HABARI NA UTANGAZAJI ARUSHA (AJTC)




Baada ya Rasimu mpya ya katiba ya kwanza kukakamilika katika chuo  cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha(A.J.T.C) wanafunzi waunga mkono wakati wa maswali ya papo kwa hapo yaliyokuwa yakiulizwa na wanafunzi na kujibiwa na mwenyekiti wa tume ya katiba hiyo Bw Oscar Samba. 

Mlezi wa wanafunzi wa chuo cha uandishi wa habari Arusha Bw Andrea Ngobole akipokea rasimu ya katiba kutoka kwa mwenyekiti wa tume ya katiba Bw Oscar Samba.
Akitoa ufafanuzi juu ya rasmu hiyo Mwenyekiti wa tume hiyo Bw.Oscar Samba alisema kuwa ni wajibu wa kila mwanafunzi kutoa na kuchangia maoni katika mchakato wa kutafuta katiba  mpya. 

Aidha aliendelea kusema kuwa kila mwanafunzi anapaswa kutoa ushirikiano wakati wakuchambua rasimu hiyo ili kujenga katiba iliyo bora na yenye kusimamia haki , jinsia na usawa kwa wanafunzi wakati wakiwa masomoni. 

Hata hivyo Bw Oscar Samba alisema kuwa kupitia mapendekezo yaliyotolewa kwenye rasmu hiyo ya katiba yanaeleza kuwa Waziri wa katiba na sheria ndiye mwenye mamlaka ya kutoa adhabu kulingana na katiba itakavyo ainisha   na sio waziri wa nidhamu kama ilivyo awali.
 
Mchakato wa  rasimu ya katiba katika Chuo cha uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha ulianza rasmi mwishoni mwa mwaka jana mwezi wa october ukiwa na lengo la kutengeneza katiba ya chuo hicho.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment