SHIRIKA LA VIWANGO NCHINI TANZANIA (TBS) LAANZISHA MSAKO KWA WAUZAJI WA NGUO ZA NDANI ARUSHA!!

Mnara wa Mwenge uliopo katikati ya Jiji la Arusha
 SHIRIKA la viwango Tanzania(TBS) limeanza oparesheni kabambe  mkoani Arusha ya
kukamata wauzaji wa nguo za ndani za mitumba ambazo zimepigwa marufuku
katika maeneo mbalimbali hapa nchini, zoezi ambalo  ni mwendelezo kwa
nchi nzima.


Akizungumza  mara baada ya zoezi hilo,Afisa viwango wa shirika hilo Bw. Paul  Manyilika alisema kuwa, oparesheni hiyo ilianzia jijini Dar es Saalamu ambapo zoezi hilo ni endelevu na  litafanyika  katika mikoa yote nchi nzima na katika zoezi hilo  wafanyabiashara sita wamekamatwa
na nguo zao baada ya kukutwa wakifanya biashara hiyo katika eneo la soko la Kibokoni lililopo mjini hapa . .

Alisema kuwa,Shirika hilo linahitaji kudhibiti uingizwaji wa nguo  za ndani za mitumba ambazo zina madhara makubwa  kwa watumiaji kutokana na kutojulikana   kiwango cha kemikali kilichotumika katika utengenezaji wa nguo hizo.

Aidha alisema kuwa, eparesheni hiyo wamekuwa wakiifanya kwa kushirikiana na jeshi la polisi ,ambapo wamekwisha ziba maeneo yote ambapo nguo hizo zinaiingilia , hivyo wanawataka wafanyabiashara wanaoendelea kuuza nguo hizo ili waweze kueleza wanapozipata.

"zoezi hili tangu limeanza limefanikiwa kwa kiasi kikubwa ,kwani wahusika wameweza kuchukuliwa hatua kali za kisheria , ikiwa ni pamoja na kuteketeza nguo hizo kwani hazitakiwi kuonekana kabisa hapa nchini."alisema Manyilika.

Alisema kuwa,matumizi ya nguo za ndani yana madhara makubwa kwa watumiaji kwani zinakuwa zimeshavaliwa na wengine, wakati kuna viwanda vikubwa hapa nchini vinavyoweza kutengeneza nguo hizo kwa usalama
zaidi na bila kuwa na madhara yoyote.

Aidha alitoa wito kwa wafanyabiashara  wanaoendelea kuuza nguo hizo kuacha mara moja kwani nguo hizo zimepigwa marufuku ,kutoka na kuleta madhara mbalimbali kwa watumiaji wake .

Kwa upande wake Mwanasheria Mkuu wa shirika hilo, Bw.Baptister Bitaho alisema kuwa, zoezi hilo ni halali kabisa na wafanyabiashara wanaofanya biashara  hizo, walishapewa notisi  ya kusitisha uuzaji wa nguo hizo masokoni , ila wengine bado wanaendelea hivyo zoezi hilo bado linaendelea na litafanyika nchi nzima.

Bitaho alisema kuwa, endapo mtu atabainika kuhusika na uuzaji wa nguo hizo ambazo zimepigwa marufuku ,adhabu yake ni shs 50 milioni hadi shs 100 milioni au kifungo cha miaka miwili jela .

POSTED BY:www.info@dirayetu.blogspot.com
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment