MOYES AKUNWA NA MATA, WENGER ASONONEKA KUDHOOFIKA KIUNGO!!


MOYES-OLD_TRAFFORD_TOUCHLINEWAKATI David Moyes akikongwa moyo na mwanzo mwema wa Mchezaji mpya Juan Mata na kurejea Uwanjani kwa Robin van Persie na Wayne Rooney kulikowapa ushindi Jana, Arsene Wenger amesononeshwa na kudhoofika kwa Kiungo cha Timu yake baada Jana kumpoteza Mathieu Flamini kwa Kadi Nyekundu na pia kuendelea kuwa nje kwa maumivu kwa Aaron Ramsey.


MOYES NA MATA, VAN PERSIE NA ROONEY
Meneja wa Manchester United, David Moyes, amesema kumsaini Juan Mata na kurejea Uwanjani kwa Robin van Persie na Watne Rooney kutoka kwenye maumivu ambako Jana kuliwapa ushindi walipoichapa Cardiff City Bao 2-0 Uwanjani Old Trafford kumeleta hali mpya kwenye Timu yao.
Van Persie Jana alirejea Uwanjani baada kuzikosa Mechi 11 na Juan Mata alicheza Mechi yake ya kwanza tangu ahamie kutoka Chelsea hivi Juzi huku Rooney akianzia toka Benchi katika Mechi yake ya kwanza tangu Januari Mosi.

Mwenyewe Mata alibainisha kufurahishwa na mapokezi yake Man United na pia kuridhika na uchezaji wake kwenye Mechi yake ya kwanza ingawa alikiri anahitaji kufanya Mazoezi zaidi baada ya kuyakosa Wiki iliyopita kwa ajili ya hekaheka za Uhamisho.
Nae Moyes amekiri kuwepo kwa Mastaa hao watatu kumeleta matumaini mapya  ingawa alisema bado ipo kazi kubwa.
Akimwongelea Mata, Moyes alisema: “Juan alifanya vyema. Alitengeneza nafasi zetu bora katika Dakika 30 za kwanza. Tutamzoea na atatuzoea. Nilitaka kuwaona yeye na Robin wakicheza pamoja. Tutamtumia katika nafasi kadhaa tofauti.”
Kuhusu Mata, Rooney na Van Persie kucheza pamoja, Moyes alisema: “Wakiwemo kwenye Timu,WENGER-PROFESA matokeo yatazidi kuwa bora!”

WENGER ASONONEKA KUDHOOFIKA KIUNGO!!
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amesononeshwa na kudhoofika kwa Kiungo cha Timu yake baada Jana kumpoteza Mathieu Flamini kwa Kadi Nyekundu na pia kuendelea kuwa nje kwa maumivu kwa Aaron Ramsey.
Jana Kiungo wao Mathieu Flamini alipewa Kadi Nyekundu walipotoka Sare ya Bao 2-2 na Southampton na hiyo inamaanisha atazikosa Mechi zijazo za Arsenal dhidi ya Crystal Palace, Liverpool na Man United.

Sare hiyo imewakosesha Arsenal kuzidi kupanda kileleni na kuwa Pointi 4 juu na hii inaweza kuwafanya waporomoke hadi Nafasi ya 3 ikiwa leo hii Man City na Chelsea zitashinda Mechi zao.
Man City wanacheza na Tottenham huko White Hart Lane na Chelsea wako kwao Stamford Bridge kuikabili West Ham na wakipata ushindi wa tofaut ya Bao 2 wataipiku Arsenal.
Pia Wenger alitoboa kuhusu kuendelea kuumwa kwa Aaron Ramsey ambae hajapona matatizo ya Paja lake.
Wenger amekiri kuwakosa Flamini na Ramsey kumedhoofisha sana sehemu ya Kiungo ya Timu yake.

LIGI KUU ENGLAND
RATIBA  YA LEO:

[Saa za Bongo]
Jumatano Januari 29
2245 Aston Villa v West Brom
2245 Chelsea v West Ham
2245 Sunderland v Stoke
2245 Tottenham v Man City
MSIMAMO:
NA
TIMU
P
GD
PTS
1
Arsenal
23
24
52
2
Man City
22
38
50
3
Chelsea
22
23
49
4
Liverpool
23
29
46
5
Tottenham
22
3
43
6
Everton
23
11
42
7
Man Utd
23
11
40
8
Newcastle
23
4
37
9
Spton
23
4
32
10
Swansea
23
-4
24
11
Aston Villa
22
-7
24
12
Norwich
23
-17
24
13
Hull
23
-7
23
14
Crystal
23
-16
23
15
West Brom
22
-5
22
16
Stoke
22
-14
22
17
Fulham
23
-28
19
18
West Ham
22
-11
18
19
Sunderland
22
-15
18
20
Cardiff
23
-23
18
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment