Waasi Syria wakubaliana kuruhusu msaada Homs!!


Wizara ya mambo ya kigeni ya Urusi, imesema kuwa serikali ya Syria na waasi wamekubaliana kuruhusu msaada wa kibinaadamu kuingizwa mjini Homs.

Kiongozi wa waasi wa Syria Bw.Ahmed Assi al-Dscharba.

Msemaji wa wizara hiyo Alexander Lukashevich aliwaambia waandishi habari mjini Moscow, kuwa yaonekana makubaliano hayo yamefikiwa.
Maelezo yake yamekuja baada ya ujumbe wa Urusi katika Umoja wa Mataifa, kusema kuwa unapinga azimio la Baraza la Usalama kuhusu hali ya kibinaadamu nchini Syria.

 Waasi wa Syria wakijiandaa kwenda kwenye mashambulizi

Wakati wa duru ya kwanza ya mazungumzo ya amani mjini Geneva, Uswisi, mwezi uliopita, wajumbe wa majadiliano kutoka pande zote walishindwa kuafikiana juu ya namna ya kuwasilisha msaada wa kibinadamu kwa watu wanaoteseka katika mji wa Homs, ambayo umezingirwa kwa siku 600 sasa.

Chanzo DW
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment