SERIKALI YATAHADHARISHA WANANCHI KUHUSU MATUMIZI MABAYA YA MAWASILIANO!!


Naibu Mkurugenzi Masuala ya Wateja kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Isaac Mrum akieleza kuhusu uhalifu wa mitandao na hatua wanazochukua katika kukabiliana na uhalifu huo ikiwepo kutoa elimu kwa umma kuhusu matumizi sahihi ya mitandao.Meneja Mawasiliano kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Innocent Mungy akiwaeleza waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu matumizi mabaya ya mawasiliano na udanganyifu katika usajili wa namba za simu za mkononi leo Jijini Dar es Salaam.


Serikali yawatahadharisha wananchi kuhusu matumizi mabaya ya Mawasiliano na udanganyifu katika usajili wa namba za simu za mkononi kwa kuwa ni kosa la jinai.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) bw. Innocent Mungy amesema kumekuwa na watu wachache wanaotumia mawasiliano pasipo kuzingatia sheria na kanuni.
 
Kumekuwa na matukio yanayoashiria kutumika kwa mitandao ya kijamii kuleta madharambalimbali kwa watumiaji ikiwemo utapeli,kulipiza kisasi, ugomvi,kuwaumiza wengine kwa mambo yasiyo na ukweli na kuvuruga kwa ujumla alisema Mungy.
 Akifafanua Mungy amesema pamoja na maendeleo chanya katika Sekta ya Mawasiliano kumekuwa na watu wachache wanaotumia simu,mitandao ya kijamii,redio,televisheni, na mawasiliano mengine kwa lengo la kuvuruga amani.
 
Kutokana na hali hiyo Mungy amesema kuwa TCRA inawakumbusha wananchi wote kwamba ni kosa la jinai kutumia mawasilano vibaya kama ilivyoainishwa kwenye sheria ya mawasiliano ya kielektroniki na Posta ( EPOCA) ya mwaka 2012.
Pia Mungy alitoa wito kwa wananchi na watumiaji wa simu za mkononi kuunga mkono juhudi za Serikali ili wananchi wote wasajili namba za simu kwa ajili ya 
kudumisha na kuendeleza amani ,usalama na kuharakisha maendeleo ya sekta hii na Taifa kwa ujumla. 

Naye Naibu Mkurugenzi Masuala ya Huduma kwa wateja toka mamlaka hiyo Bw. Isaac Mruma amesema ni vyema wananchi wakazingatia matumizi sahihi ya mawasiliano kwa maslahi mapana na Taifa.
 
Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta (EPOCA) mwaka 2010, kifungu cha 131 imeainisha kuwa ni kosa la jinai kutumia au kuwezesha kutumika kwa namba ya simu isiyosajiliwa na adhabu yake ni faini ya shilingi laki tano (Tsh. 500,000) au kifungo cha miezi mitatu kwa atakayekiuka sheria hii
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment