SAKATA LA PROF. MUHONGO: kikwete kutoa uamuzi-Ikulu!!

 

KURUGENZI ya Mawasiliano ya Rais Ikulu Dar es Salaam, imesema Rais Jakaya Mrisho  Kikwete atatoa uamuzi wake juu ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo aliyewekwa kiporo baada ya kuhusishwa kwenye sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow.

Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu Bw. Salva Rweyemamu aliyasema hayo Dar es Salam jana wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari na kuongeza kuwa Rais Kikwete atatoa uamuzi wake baada ya uchunguzi kukamilika.

Alisema pamoja na Bunge kutoa maazimio yake ili yaweze kutekelezwa na mamlaka ya uteuzi, taratibu za kumwajibishan mtumishi wa umma na kiongozi wa kisiasa unatofautiana ndiyo maana Prof. Muhongo yupo hadi sasa.

Akizungumzia suala la wabunge kukwerwa na misamaha ya kodi, Bw. Rweyemamu alisema hata Serikali haipendezwi na jambo hilo kwani bila kukusanya kodi hakuna maendeleo.

"Misamaha hii inawachukiza wabunge kwa sababu bado hawajapitisha sheria ya kuifuta misamaha hiyo...mwaka 2014, Serikali ilipeleka Muswada wa Sheria bungeni ili kuifuta misamaha yote ya kodi lakini wabunge walikataa kuipitisha.

"Nashangaa kuona baadhi ya wabunge kukerwa na misamaha ya kodi wakati wao ndiyo waliokataa kupitisha muswada wa kufuta misamaha hiyo bungeni," alisema Bw. Rweyemamu.

Juzi Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), iliitaka Serikali ifanye kila linalowezekana ili kupunguza misamaha ya kodi ambayo mwaka wa fedha 2013/14 ilipaa kwa sh. bilioni 340 kutoka sh.trilioni 1.48 hadi sh. trilioni 1.82 mwaka 2014.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment