WANANCHI WA ZAMBIA KUPIGA KURA LEO KUMCHAGUA RAIS MPYA!!


Hatimaye leo wananchi wa Zambia wanapiga kura kumchagua Rais wa nchi hiyo kufuatia kifo cha Rais wa nchi hiyo Michael Sata aliyefariki dunia Oktoba mwaka jana.

Chama tawala cha Patrioyoc Front kinauhakika wa kushinda katika uchaguzi huo licha ya kukabiliwa na upinzani mkali kutoka upinzani.

Waangalizi wa kikanda katika uchaguzi huo wanasema wameridhishwa na maandalizi ya zoezi zima la upigaji kura.
Uchaguzi huo unatarajiwa kuwa na upinzani mkali kati ya Edgar Lungu anayegombea nafasi hiyo kupitia chama tawala na mpinzani wake Hakainde Hichilema kutoka United Party for National Development.
Wagombea wote katika nafasi hiyo ya Urais wakati wakijinadi wameahidi kuimarisha mfumo wa elimu nchini humo, kutengeneza ajira. Huku wapiga kura wao wakitumaini kuwa wanasiasa hao watatimiza ahadi zao. 
Ikiwa ni miaka 50 toka nchi hiyo ilipojipatia uhuru, Zambia imekuwa imara na imeendelea na msimamo wake wa kufanya uchaguzi tangu kumalizika kwa siasa za chama kimoja nchini humo.
Hata hivyo mshindi katika uchaguzi huo wa leo atatumikia kipindi cha miezi 18 iliyobakia, katika awamu aliyoiacha marehemu Michael Sata, wakati nchi hiyo ikijiandaa kufanya uchaguzi mkuu mwakani 2016.
Vituo vya kupigia kura vitafunguliwa kuanzia saa 12 kamili asubuhi na kufungwa saa 12 jioni. Tume ya Uchaguzi nchini Zambia imesema zoezi la uhesabuji kura linatarajiwa kuanza muda mfupi tu baada ya zoezi la upigaji kura kukamilika huku matokeo yakitarajiwa kutangazwa katika kipindi cha saa 48.
Chanzo:BBC
 

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment