SUMATRA YAAMRIWA KUSHUSHA BEI ZA NAULI!!

Mwenyekiti wa Chama cha Kutetea Abiria (Chauka), Hassan Mchanjama (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar
Chama  cha Kutetea Abiria (Chakua) kimeitaka Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Ardhini Sumatra kukutana na wadau kujadili punguzo la nauli kutokana na kuendelea kuporomoka kwa bei ya mafuta.
 
Mwenyekiti wa Chakua, Hassan Mchanjama alisema mafuta yamepungua bei kutoka Sh2,200 hadi Sh1,768 kwa lita moja ya petroli huku diseli ikishuka hadi kufikia Sh1,708 kwa lita.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mchanjama alisema wanapendekeza nauli ishuke kwa asilimia 25 kwa usafiri wa daladala inayoenda masafa ya chini ya kilometa 10.
Alifafanua kuwa kwa nauli ya sasa ya Sh400, kushuka kwa bei ya mafuta kutafanya nauli pia ishuke hadi kufikia Sh300 na kwa upande wa mabasi ya mikoani nauli ishuke kutoka Sh40,000 hadi Sh30,000.
Alifafanua kuwa kushuka kwa nauli za mabasi kutasababisha pia kushuka kwa bei ya bidhaa mbalimbali ikiwemo chakula na mazao mengine ya biashara.
Chama hicho kimemuomba pia Waziri wa Uchukuzi, Samweli Sitta aingilie kati na kuiagiza Sumatra isikilize kilio cha wananchi kwa kuitisha mkutano ili kushusha nauli kama ilivyokuwa mwaka 2009 baada ya mafuta kupungua bei nauli zikapungua.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment