![]()  | 
| Mwenyekiti wa Chadema taifa, Freeman Mbowe akiwa pamoja na Mbunge Joshua Nassari (kushoto) na Godbless Lema (kulia) katika moja ya mikutano ya chama hicho. Picha na Maktaba | 
Majimbo hayo ni jimbo la Arusha mjini, mbunge 
wake, Godbless Lema, Jimbo la Arumeru Mashariki, mbunge Joshua Nassari 
na Jimbo la Karatu mbunge, Mchungaji Israel Natse ambapo tayari kuna 
   wanachama wa chama hicho, wameanza kutangaza nia   za kuwang’oa 
wabunge hao.
                
              
Akizungumza na mwandishi wetu leo, Katibu wa Chadema 
mkoa wa Arusha, Calist Lazaro alisema, maagizo anayoyatoa ni kutekeleza 
utaratibu ambao umetolewa na Kamati Kuu ya chama hicho,kuhusiana na 
uchaguzi mkuu ujao.
                
              
“Naomba hapa ieleweke kuwa hatuzuwii mtu kugombea 
lakini tunataka afuate taratibu ili kuzuia vurugu na kama mtu akikiuka 
sasa ina maana atakuwa amepoteza sifa”alisema Lazaro.
                
              
Lazaro alisema nia ya agizo hilo ni kuondoa vurugu
 na mpasuko ndani ya chama kabla ya wakati muafaka wa kutangaza nia na 
kuanza kampeni haujafika, lakini kwa majimbo yaliyo na wabunge wa CCM, 
wagombea wanaruhusiwa kutangaza nia.
                
              
Alisema  chama hicho,  kitatoa ratiba ya uchaguzi 
karibuni na  fomu za kugombea  nafasi mbali mbali zitapatikana katika 
ofisi za chama hicho, katika ngazi zote ila kwa maeneo yenye wabunge na 
madiwani wa chadema, fomu zitapokelewa bila kutangaza nia na kuanza 
kampeni.
                
              
Tamko hilo limekuja kukiwa na mpasuko mkubwa ndani
 ya Chadema katika majimbo hayo matatu, kutokana na idadi kubwa ya 
makada wa chama hicho, kuanza kunyemelea majimbo hayo.

0 comments:
Post a Comment