|  | |
| Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hoteli ya Serena, jijini Dar es Salaam jana. | 
Maalim Seif aliyewania urais wa Zanzibar katika 
uchaguzi huo na kushindwa ikiwa ni mara ya tano na wagombea wa CCM, 
alitoa tuhuma hizo jana alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar 
es Salaam akisema wapigakura hao wasiostahili, bado wapo kwenye Daftari 
la Kudumu la Wapigakura la Zanzibar.
                
              
Maalim Seif ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF, 
alikuwa akizungumzia utafiti wa Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa 
Zanzibar uliofanywa kati ya Agosti 2014 hadi Machi 2015. Alieleza pia 
kwa nini hakulalamika wakati huo na badala yake akakubali matokeo.
                
              
Kwa nini alikubali matokeo?
                
              
“Ni ukweli usiopingika kwamba uchaguzi huo ulikuwa
 na mapungufu lukuki lakini mawakala wetu hawakuwa na vithibitisho, 
hatukuweza kupinga matokeo yale kwa sababu hatukuwa na uthibitisho 
wowote.”
                
              
Aliongeza, “Hivi unaweza kusema matokeo siyo ya 
haki wakati huna uthibitisho? Lakini utafiti huu umeweka wazi mambo yote
 yaliyofanywa nyuma ya pazia kwenye uchaguzi uliopita, kwa hiyo sasa 
tuna uthibitisho wa kutosha.”
                
              
Kiongozi huyo alisema endapo kasoro hizo 
zikifanyiwa kazi, Rais wa sasa, Dk Ali Mohamed Shein ajiandae 
kisaikolojia kuwa makamu wa rais wakati yeye akiwa Rais baada ya 
uchaguzi ujao.
                
              
Kasoro za uandikishaji
                
              
Kwa mujibu utafiti huo, ZEC iliandikisha katika 
daftari hilo wapigakura wenye umri chini ya miaka 18, ambao si wakazi 
katika maeneo waliojiandikisha na waliotumia majina na picha ambazo siyo
 zao.
                
              
Alisema licha ya baadhi ya watu hao kuwa marehemu 
na wengine wasiokuwa na sifa, bado hawajafutwa kwenye daftari hilo tangu
 2010 na majina yao yatatumika kupiga kura mwaka huu.
                
              
Akizungumza kwa kujiamini huku akitabasamu, Maalim
 Seif alisema utafiti huo unaonyesha kuwa kuna zaidi ya watu 10,000 
ambao waliandikishwa kinyume na sheria na kwamba walipiga kura katika 
uchaguzi wa mwaka 2010.
                
              
Akitoa mfano huku akirejea utafiti huo, Maalim 
Seif alidai kwamba katika Jimbo la Donge, ZEC iliandikisha watoto 463 
ambao hawajafikisha umri wa miaka 18 na kwamba walipiga kura.
Katika matokeo ya Uchaguzi Mkuu 2010, Zanzibar mgombea urais wa 
CCM, Dk Ali Mohamed Shein alipata kura 179,809 sawa na asilimia 50.1 
wakati Maalim Seif wa CUF alipata kura 176,338 sawa na asilimia 49.1.
                
              
Maalim Seif aliwataja na kuonyesha picha za watu aliodai waliandikishwa kinyume na sheria na maeneo wanayotoka.
                
              
“Hii ni sehemu ya rafu zilizofanywa na ZEC ambazo 
tumezibaini kwenye utafiti, tuna ushahidi wa kila aina, tunajua majina 
yao, wanapoishi, vitambulisho vyao na picha zao,” alisema.
                
              
Utafiti wenyewe
                
              
Mkuu wa Kitengo cha Sera, Utafiti na Mafunzo wa 
CUF, Hassan Jani Masoud alisema makosa yaliyoonekana katika uandikishaji
 wa daftari hilo yanarudisha nyuma demokrasia.
                
              
Alisema ukiangalia sura za watoto walioandikishwa 
kwenye daftari unagundua kwamba ZEC ilidhamiria kuisaidia CCM kwa 
gharama zozote.
                
              
“Ni watoto wadogo lakini walivyoandikishwa 
wameonyesha kwamba wamefikisha umri wa miaka 18, hii ni hatari,” alisema
 na kuongeza:
“Kuna wale walioandikishwa kwa zaidi ya mara moja, unakuta picha ya mtu mmoja lakini imepigwa kwa nyakati tofauti na majina yanatofautiana.”
                
              “Kuna wale walioandikishwa kwa zaidi ya mara moja, unakuta picha ya mtu mmoja lakini imepigwa kwa nyakati tofauti na majina yanatofautiana.”
Kinachofanyika sasa
                
              
Maalim Seif alisema shughuli ya uandikishaji wa 
Daftari la Kudumu la Wapigakura itaanza Mei 16 hadi Juni 28, mwaka huu 
na imebainika kwamba yaliyojitokeza katika uchaguzi uliopita yatarudiwa.
                
              
“Hivi tunavyozungumza kunaendelea zoezi kubwa la 
kuandaa wapigakura haramu ili waweze kuja kuandikishwa,” alidai na 
kuongeza kuwa maandalizi hayo yanahusisha Idara ya Usajili wa 
Wazanzibari ambao ndiyo hutoa vitambulisho vya Mzanzibari, wakuu wa 
mikoa na wilaya, masheha na sekretarieti ya ZEC na vikosi vya ulinzi na 
usalama.
                
              
Alisema kambi moja ya jeshi Zanzibar inatumika 
kuandikisha mamia ya vijana ambao wanapewa vitambulisho vya Mzanzibari 
Mkaazi ili waje waandikishwe kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura.
                
              
“Vijana hao wamekuwa wakipelekwa kwenye kambi hiyo
 kwa magari maalumu katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita na wiki 
iliyopita wameitwa na kupewa vitambulisho vya wakaazi,” alidai.
Alidai kuwa katika majimbo mbalimbali ya Unguja na Pemba, vijana
 wanaofikia 20,000 wameandikishwa na kupewa vitambulisho na miongoni 
mwao wapo watoto walio chini ya umri wa miaka 18.
                
              
Upande wa ZEC
                
              
Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha hakupatikana 
jana kuzungumzia madai hayo licha ya kupigiwa simu zaidi ya mara tatu na
 gazeti hili.
                
              
Hata aliyetajwa kuwa Mkurugenzi wa ZEC alipopigiwa
 simu yake ya mkononi, alipokea na kujibu kwamba yeye si mkurugenzi wa 
tume hiyo.
                
              
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa
 Zanzibar, Mohammed Aboud Mohammed alipopigiwa simu alisema: “Nipo 
kwenye kikao” na kukata simu.
                
              
Alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno kwenye simu 
yake na kuulizwa kuhusu hali hiyo, Aboud alijibu: “Nipo kwenye BLW 
(Baraza la Wawakilishi) kwenye kamati ya uongozi.”
                
              
Maagizo ya CUF
                
              
Maalim Seif  alisema ili Uchaguzi Mkuu ujao uwe 
huru na amani na ili kuiepusha nchi na vurugu, chama hicho kimetoa 
maagizo tisa ambayo SMZ na ZEC wanatakiwa kuyachukua.
                
              
Maagizo hayo ni pamoja na “Wapigakura haramu wote 
waliopatiwa vitambulisho vya Mzanzibari mkazi kinyume na sheria watakiwe
 kuvisalimisha na wasiandikishwe katika Daftari la Kudumu la Wapigakura.
                
              
Agizo jingine ni watu wote wenye haki ya kupatiwa 
vitambulisho wapewe kabla ya uandikishaji wapigakura ili waweze kutumia 
haki yao ya kupiga kura.
                
              
Vilevile, vikosi vya jeshi na Idara Maalumu ya SMZ ziache kutumiwa kisiasa na kwenda kinyume na sheria zinazoongoza kazi zao.
                
              
Ofisi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tawala za 
Mikoa na Idara Maalumu za SMZ) iache kuwatumia wakuu wa mikoa, wilaya na
 masheha katika kusajili wapigakura haramu kwa kuwapatia vitambulisho.
CUF pia imeitaka pia Idara ya Usajili wa Mzanzibari iache 
kutumika kisiasa kwa kusajili watu wasio Wazanzibari, watoto wadogo na 
watu wanaotoka nje ya majimbo yao kwa lengo la kuisaidia CCM.
                
              
Chama hicho kimelitaka Jeshi la Polisi lisikubali 
kutumiwa kinyume na sheria kuwalinda wapigakura haramu wanapopelekwa 
kwenda kujiandikisha
                
              
Chama hicho pia kimetaka Daftari la Wapigakura 
lifanyiwe uhakiki kwa mfumo wa kielektroniki unaotumia alama za mwili 
(BVR) ili kuwafuta waliosajiliwa zaidi ya mara moja na kuwaondoa 
waliofariki na watoto chini ya umri wa miaka 18.
                
              
Agizo jingine ni kuwa sekretarieti ya ZEC ifanyiwe marekebisho ili iwe huru isiyojiegemeza kwa CCM.
                
              
Pia, CUF imetaka ZEC ikatae kutumiwa na CCM katika suala la ukataji wa mipaka ya majimbo ya uchaguzi.
                
              
Maridhiano
                
              
“Pamoja na matatizo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010
 tuliweza kuvuka salama kupitia misingi madhubuti ya maridhiano ambayo 
tuliyaasisi mimi na Rais mstaafu, Aman Karume,” alisema na kuongeza: 
“Sisi tulitekeleza wajibu wetu ni imani yangu kwamba Rais Jakaya Kikwete
 na Rais Ali Mohamed Shein nao watafanya wajibu wao ili kuepuka 
kuturudisha kule tulikotoka.
                
              
“Naomba niwakumbushe wenzangu kwamba wimbi la 
mabadiliko linapofikia wakati wake huwa halizuiliki tena, CCM isitarajie
 kuendelea kubakia madarakani kwa kutumia njia za hadaa, hujuma, 
udanganyifu, nguvu na vitisho.
                
              
Kwa nini asiwaache wengine?
                
              
Maalim Seif alipoulizwa kama yuko tayari kuwaachia
 wengine kuwania nafasi ya urais katika SMZ kupitia chama hicho na yeye 
kupumzika, alisema: “Sijawahi kuwakataza wanachama wa CUF kuwania nafasi
 ya urais, mimi nimekuwa nikijitokeza kuwania na wengine wajitokeze 
kuwania na hii ndiyo demokrasia.”
                
              
Alisema wanachama wa chama hicho wana haki sawa ya
 kugombea nafasi yoyote ya uongozi ikiwamo urais... “Sasa kama 
hawajitokezi hilo si tatizo langu, mimi nimekuwa nikijitokeza.”
                
              
Uhakiki wa ZEC
Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa CUF, Ismail Jussa Ladhu alisema 
chama hicho kinaendelea na msimamo wake wa kutaka uhakiki ZEC ufanywe na
 kampuni za kimataifa.
                
              
“Tunaamini kampuni kutoka nje itakuwa huru na itatenda haki katika jambo hili tofauti na kampuni ya hapa ndani,” alisema.
                
              
Alisema kasoro hizo zikiondolewa, Dk Shein ajiandae kisaikolojia kuwa makamu wa kwanza wa Rais wa SMZ
                
              
“Kasoro zilizopo zikirekebishwa tunachukua nchi katika Uchaguzi Mkuu ujao, Dk Shein ajiandae kutupisha,” alisema.
                
              
Kwa nini utafiti Zanzibar tu?
                
              
Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed 
Mazrui alisema ulifanywa Zanzibar pekee yake ili kupata matokeo kabla ya
 Uchaguzi Mkuu.
                
              
 “Tumefanya upande wa Zanzibar kwa sababu kama 
tungefanya Tanzania nzima gharama zingekuwa kubwa na utafiti ungechukua 
muda mrefu,” alisema.
                
              
Alisema lengo lilikuwa kukiwezesha chama kuchukua hatua zinazostahili.
                
              
Kauli ya CCM
                
              
Akizungumzia madai ya Maalim Seif, Naibu Katibu 
Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alisema tuhuma hizo ni za uzushi na 
wala hazina ukweli wowote.“(CUF)  wanafahamu tupo kwenye maandalizi ya 
Uchaguzi Mkuu kwa hiyo wanaanza kujenga hofu za makusudi kwa watu na 
kuipaka matope CCM kwa tuhuma za uongo ili watakaposhindwa waseme 
tumewaonea,” alisema Vuai na kuongeza:
                
              
“ZEC ina wawakilishi saba, wawili wanatoka CUF 
ambao waliwapendekeza wenyewe kwa ajili ya kuhakikisha kunakuwa na 
uchaguzi huru na haki, sasa wanacholalamikia ni nini! Wanataka kusema 
wawakilishi wao wanawageuka?”Alisema chama hicho hakitakiwi kuilalamikia
 CCM badala yake wailalamikie tume hiyo kwani ndiyo iliyopewa dhamana ya
 kusimamia uchaguzi.
0 comments:
Post a Comment