Mwenyekiti wa bodi ya ushauri ya
 kupambana na maswala ya rushwa katika umoja wa Africa kutoka Ghana 
Mh.Daniel Batidam akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo 
mbalimbali vya habari jijini Arusha  katika ukumbi wa mikutano AICC 
katika kuangalia jinsi gani wataweza kupambana na kufikia malengo ya 
kutokomeza Rushwa ndani ya Bara La Africa.(Habari picha na Pamela Mollel
 wa jamiiblog)
Makamu Mwenyekiti bodi ya ushauri ya kupambana na maswala ya rushwa katika umoja wa Africa Mh.Florince Ziyambi kutoka Zimbabwe
Muongoza vikao kutoka Kenya Mh.John Tuta akitambulisha wajumbe
Mwaandishi wa habari Merry Mwita akiuliza maswali katika mkutano huo
Muonekano ndani ya ukumbi
                                                                 Picha ya Pamoja ya 
Wakuu wa taasisi za kuzuia Ruswa
 barani Africa
Wakuu wa taasisi za kuzuia Ruswa
 barani Africa wamekutana  katika ukumbi wa mikutano AICC katika 
kuangalia jinsi gani wataweza kupambana na kufikia malengo ya kutokomeza
 Rushwa ndani ya Bara La Africa.
Wakuu hao ambao ni wajumbe wa 
Bodi ya Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa barani Afrika AUABC 
iliyopo chini ya jumuia ya muungano wa nchi za Afrika ambapo mwenyekiti 
wa Taasisi ya AUABC Jaji Daniel Batidam amesema kuwa wanatarajia kwa 
mkutano huu utasaidi kupunguza makali ya Ruswa ndani ya bara hili.
Amesema kuwa kiwango kikubwa 
wanaangalia jinsi gani wataweza kuondoa ruswa katika taasisi za jamii 
kwa maana ndio zinazochangia kwa kiasi kikubwa maenbdeleo ya nchi zetu 
za kiafrika.
Pamoja na hayo amesema kuwa 
tatizo kubwa la Rushwa ndani ya bara la Afrika ni mfumo uliopo ambao 
unakuwa unaweka mianya ya rushwa pamoja na hayo alisisistiza kwa 
wananchi kuacha kutoa rushwa ili kuiondoa kabisa.
Bodi hiyo imeundwa na watu 11 kutoka nchi mbalimbali barani Africa
0 comments:
Post a Comment