FUATILIA UZINDUZI WA MFUKO WA MAENDELEO KWA DARASA LA MOUNT UDZUNGWA HAPA.

Pichani ni Mkurugenzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha  Bwana JOSEPH KAGIE MAYAGILA(katikati) Bi Hellen Bampale (mwanafunzi wa darasa kushoto) na Mwalim mlezi Bi.Neema Mwaipela wakiskiliza Risala ya Darasa la Mount UDZUNGWA.

 Mshereheshaji mkuu katika shuguli hiyo Bwana AGAPE MSUMARI ambaye alikuwa kivutio kikubwa katika shuguli hiyo akitoa maelezo ya jumla kwa wageni waalikwa.



Msomaji wa taarifa ya habari katika darasa hilo Bi Janeth Sisu akisoma taarifa ya habari kuonyesha mgeni rasmi nikwajinsi gani darasa hilo lilivyojikita katika nyanja  ya uandikaji wa habari na usomajiti.

Wanafunzi wa darasa la mount Udzungwa wakifuatilia kwa makini shuguli nzima inavyokwenda.

Rais wa Serikali ya wanafunzi Bwana GEORGE SILANGE (kulia) akifuatilia kwa makini matukio mazima ya darasa hilo.




Dj na muandaaji mkuu wa matangazo Bwana Azizi Mwinuka akifanya vitu vyake katika shuguli hiyo.

Fundi mitambo wa darasa la Mount Udzungwa Bwana Rajabu Sultani (aliyekaa) akihakikisha shuguli nzima inaenda sawa.

Wanafunzi wa darasa la mount Udzungwa wakifuatilia kwa makini shuguli nzima inavyokwenda.

Mwalimu wa Darasa la Mount Udzungwa Bwana Andrea Ngobole akisalimia wageni waalikwa.

Msomaji wa habari za michezo Bi Mercy Rodrick akisoma habari za michezo kuonyesha ni jinsi gani wanawake wanavyokimbiza habari za michezo


Bi Jeska Mhoka akisoma risala mbele ya mgeni Rasm.

Mkurugenzi wa Chuo hicho Bwana JOSEPH KAGIE MAYAGILA akipokea risala fupi ilyosomwa na Bi Jeska Mhoka.


 Mkurugenzi wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Arusha Bwana Joseph Kagie Mayagila akijibu risala ilyosomwa kwake na mmoja wa wanafunzi wa darasa hilo Bi Jeska Mhoka


Mwalimu wa taaluma katika Chuo hicho Bwana Adson Kagie Mayagila akiskiliza kwa makini malengo ya darasa hilo.



Keki ilyoandaliwa na darasa hilo pamoja na Shanpein kwaajili ya uzinduzi wa mfuko wa maendeleo wa darasa hilo.


Mkurugenzi wa Chuo hicho akikata keki hiyo kufungua rasmi mfuko wa maendeleo wa darasa hilo


Hawa ni washehereshaji walioipamba shuguli nzima ya siku hiyo wakionyesha vipawa vyao katika kuendesha shuguli mbalimbali katika jamii.


Picha ya pamoja ilyojuisha wageni rasmi katika shuguli hiyo na wanafunzi wa darasa la Mount Udzungwa.


 Katika  uzinduzi huo wa mfuko wa maendeleo kwa darasa hilo mkurugenzi wa chuo hicho Bwana Joseph Kagie Mayagila aliwataka wanafunzi hao kujikita zaidi katika sekta ya ujasriamali kwani  ndiyo njia pekee yakumkwamua mtu katika hali duni ya maisha.

Hatahivyo Bwana Mayagila aliwataka wanafunzi hao kupenda kujisomea vitabu mbalimbali vya ujasriamali kwani kwakupia vitabu hivyo zipo mbinu nyingi zinazopatikana huko ili kuweza kugundua njia mbadala za kiushindani katika biashara.

"Kunambinu nyingi sana zakuweza kukuinua kibiashara katika ujasriamali hivyo pendeni kujisomea vitabu mbalimbali vya ujasriamali ili kujiongezea elimu zaidi tofauti na ile mnayosoma huku mkiomba ushauri kwa waalimu wenu wa somo la ujasriamali"alisema.

Picha na Habari kwahisani ya www.info@dirayetu.blogspot.com




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment