
Hii ni Mechi ya kwanza kati yao ya VPL,
Ligi Kuu Vodacom na Simba wapo kileleni mwa Ligi hiyo kwa kushinda Mechi
5 na Sare 3 wakiwa na Pointi 18 wakati Yanga wameshinda Mechi 4 Sare 3
na kufungwa 1 na wana Pointi 15.
Simba, ambao wako chini ya Kocha
Abdallah Kibaden, walikuwa mafichoni huko Bamba Beach, Kigamboni, Dar es
Salaam wakinoa Mfumo wao wa 4-4-2 ambao wanatarajiwa kuutumia leo hii.
Yanga, chini ya Kocha Ernie Brandts
kutoka Holland, wao walijichimbia Visiwani Pemba, wakjizoeza na
Fomesheni yao ya 4-3-3 ambayo huwafanya washambulie muda wote.
REKODI:
LIGI KUU: Ushindi Yanga 37 Simba 32 Sare 31
UBINGWA: Yanga 23 Simba 18
Wakiongea kabla Mechi hii, Kocha wa
Simba, Kibaden, ameripotiwa kutamka kuwa Timu yake imejitayarisha vyema
na ipo kwenye hali ya ushindi.
Nae Brandts wa Yanga amesema Wachezaji wake wote wako fiti na wako tayari kuwavaa wapinzani wao.
DONDOO MUHIMU:
-BEI ZA TIKETI:
-Sh. 5,000 Viti vya rangi ya kijani [Viti 19,648]
-Sh 7,000 Viti vya rangi ya bluu
-Sh 10,000 Viti vya rangi ya chungwa
-Sh 15,000 VIP C
-Sh 20,000 VIP B
-Sh 30,000 VIP A [Viti 748]
-TIKETI KUUZWA SIKU MOJA.
-VITUO MAUZO YA TIKETI: Shule
ya Sekondari Benjamin Mkapa, Sokoni Kariakoo, Mgahawa wa Steers ulioko
Mtaa wa Ohio/Samora, Oilcom Ubungo, Kituo cha Mafuta Buguruni, Dar Live
Mbagala, Uwanja wa Uhuru, na BMM Salon iliyoko Sinza Madukani.
-REFA: Israel Nkongo [Dar es Salaam]
-MAREFA WASAIDIZI: Hamis Changwalu [Dar es Salaam] na Ferdinand Chacha [Bukoba]
-REFA wa AKIBA: Oden Mbaga [Dar es Salaam].
-KAMISHNA: John Kiteve [Iringa]
-MTATHMINI WA WAAMUZI: Stanley Lugenge [Njombe]
Mara ya mwisho Timu hizi kukutana ni
hapo Mei 18 katika Mechi ya mwisho ya Msimu wa VPL wa 2012/13, Msimu
ambao Yanga aliibuka Bingwa, na katika Mechi hiyo Simba alinyukwa Bao
2-0 kwa Bao zilizofungwa na Didier Kavumbagu na Hamisi Kiiza.
Katika Mechi hiyo, Supastraika, Mrisho Ngassa, alivaa Jezi ya Simba lakini safari hii, Ngassa atavaa Jezi ya Yanga.
VPL: MECHI ZA YANGA NA SIMBA LIGI MSIMU HUU 2013/14
YANGA P:8 W:4 D: 3 L: 1 |
SIMBA P: 8 W:5 D:3 L:0 |
Yanga 5 Ashanti 1 |
Rhino Rangers 2 Simba 2 |
Yanga 1 Coastal Union 1 |
JKT Oljoro 0 Simba 1 |
Mbeya City 1 Yanga 1 |
Simba 2 Mtibwa Sugar 0 |
Tanzania Prisons 1 Yanga 1 |
Simba 6 Mgambo JKT 0 |
Azam FC 3 Yanga 2 |
Simba 2 Mbeya City 2 |
Yanga 1 Ruvu Shooting 0 |
JKT Ruvu 0 Simba 2 |
Yanga 2 Mtibwa Sugar 0 |
Ruvu Shooting 1 Simba 1 |
Kagera Sugar 1 Yanga 2 |
Simba 1 Tanzania Prisons 0 |
VIKOSI VINAWEZA KUWA:
YANGA [Mfumo 4-3-3]:
Ally Mustapha 'Barthez', Mbuyu Twite, David Luhende, Nadir Haroub
'Cannavaro', Kelvin Yondani 'Cotton', Athuman Idd 'Chuji', Haruna
Niyonzima, Frank Domayo 'Chumvi' , Didier Kavumbagu, Mrisho Ngassa,
Hamis Kiiza.
SIMBA [Mfumo 4-4-2]:
Abel Dhaira, Nassor Said, Rashid Issa, Kaze Gilbert, Joseph Owino, Jonas
Mkude, Abdulhalim Humuod, Ramadhan Singano, Haroun Chanongo, Amisi
Tambwe, Betram Mombeki.
POSTED BY:www.info@dirayetu.blogspot.com
0 comments:
Post a Comment