LIGI KUU ENGLAND: FULHAM YAPIGA 4, MOURINHO KWA ‘PILATO!’

KWENYE Mechi pekee ya BPL, Ligi Kuu England, Jana Usiku Fulham waliichapa Crystal Palace Bao 4-1 na Wachezaji wao Pajtim Kasami na Steve Sidwell kufunga Bao 2 safi sana ambazo, bila shaka, zimo kwenye kinyang’anyiro cha Goli la Msimu.
Adrian Mariappa ndie aliwapa Crystal Palace bao lao pekee kwa kichwa lakini Kasami na Sidwell wakaigeuza Mechi hiyo kabla ya Haftaimu.
Kipindi cha Pili, kichwa cha Dimitar Berbatov na tikitaka ya  Philippe Senderos kiliwapa Fulham ushindi mnono.

Magoli:
Crystal Palace 1
-Mariappa Dakika ya 7
Fulham 4
-Kasami Dakika ya 19
-Sidwell 45
-Berbatov 50
-Senderos 55

BPL2013LOGOHiki ni kipigo cha 7 kwa Crystal Palace katika Mechi zao8 za Ligi na wapo Nafasi ya 19 ikiwa ni Nafasi moja toka mkiani na hii ni presha kubwa kwa Meneja wao Ian Holloway.
Kwa Fulham, huu ni ushindi wao wa pili mfululizo kwenye Ligi na umewapandisha hadi Nafasi ya 14 na kumpa ahueni Meneja wao Martin Jol aliekuwa akisakamwa.
Jose Mourinho: afunguliwa Mashitaka na FA

Meneja wa Chelsea Jose Mourinho amefunguliwa Mashitaka na FA, Chama cha Soka England, kwa utovu wa Nidhamu kwenye Mechi ya ushindi wa Klabu yake walipoichapa Cardiff City Bao 4-1 Jumamosi iliyopita Uwanjani Stamford Bridge.
Kwenye Mechi hiyo, Refa Anthony Taylor alimwondoa Mourinho toka kwenye Benchi la Ufundi baada ya kulalamikia upotezaji muda waa Wachezaji wa Cardiff City na Meneja huyo akalazimika kuitazama Mechi hiyo kwa Dakika 20 zilizobaki akiwa Jukwaa la Washabiki.
Kabla kufunguliwa Mashitaka, Mourinho alisema: “Sielewi kwa nini Refa amenizuia kufanya kazi yangu!”
Mbali ya Mourinho kupewa Kadi Nyekundu, pia kwenye Mechi hiyo kulikuwa na utata mkubwa pale Bao la kusawazisha la Chelsea kukubaliwa kinyume na Sheria za FIFA kwani  Kipa wa Crystal Palace Marshall alikuwa ameudaka Mpira na aliudunda chini na Eto’o kuudokoa na baadae kumfikia Hazard aliefunga.
Kwa mujibu wa FIFA, tukio hilo lilipaswa kuamuliwa ni faulo dhidi ya Chelsea.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment