SIR ALEX FERGUSON AZINDUA KITABU KINACHOELEZEA HISTORIA YA MAISHA YAKE!!


ALEX_FERGUSON-MY_AUTOBIOGRAPHYSir Alex Ferguson leo amezindua Kitabu cha maisha yake na miongoni mwa mengi yaliyoibuliwa humo ni sababu zilizofanya David Beckham kuondoka Manchester United.
Katika Kitabu hicho kiitwacho ‘Alex Ferguson: My Autobiography’,
Ferguson amesema ilifika hatua Beckham kujiona ‘yu mkubwa kupita Meneja!’ na walianza kukorofishana wakati Beckham alipopondwa kwa kucheza vibaya wakati Man United ilipofungwa na Arsenal Mwaka 2003 kwenye FA CUP.
Ferguson ameeleza: “Ikifika Dakika Mchezaji wa Manchester United anajiona yuko mkubwa kupita Meneja, lazima aondoke. David alijiona yu mkubwa kupita Alex Ferguson.”

MAMBO MUHIMU YANAYOELEZEWA HUMO:
-Wayne Rooney alipoteza ukali wake Msimu uliopita ambao ndio ulikuwa wa mwisho kwa Ferguson kwa kuwa hakuwa fiti.
-Aliigomea England mara mbili kuwa Meneja wake
-Cristiano Ronaldo ndie Mchezaji mwenye Kipaji kikubwa kupita yeyote aliewahi kumwongoza na anamuita ‘Mchawi.’
-Alimwambia Ronaldo yuko tayari kumpiga risasi kuliko kumuuza kwa Real Madrid
-Kitu kigumu katika mwili wa Roy Keane ni ulimi wake na alikuwa na kauli mbaya kupita mfano!
-England hawawezi kutwaa Kombe la Dunia mpaka wapate Wachezaji wenye kipaji kama Brazil

Ferguson pia ameandika kuwa alikerwa na maisha ya Beckham ya kusaka umaarufu baada ya kumuoa Mwimbaji wa Kundi la Spice Girls Victoria Adams.
Ferguson amesema: “David alikuwa ndie Mchezaji pekee niliemwongoza aliechagua umaarufu, alietaka kujulikana nje ya Gemu. Sikusikia vizuri na maisha hayo ya umaarufu.”
Beckham, ambae akiwa na Man United alinyakua Ubingwa wa Ligi mara 6, FA CUP 2 na UEFA CHAMPIONZ LIGI moja, aliuzwa kwa Real Madrid Mawaka 2003 kwa Pauni Milioni 25.
Katika Miaka yake 26 akiwa na Man United, Sir Alex Ferguson alitwaa Makombe 38 na kuongoza baadhi ya Majina makubwa kwenye Soka wakiwemo Beckham, Eric Cantona, Cristiano Ronaldo, Peter Schmeichel, Bryan Robson, Roy Keane, Jaap Stam na Ruud Van Nistelrooy.
Ferguson alistaafu Man United Mwezi Mei na nafasi yake kuchukuliwa na David Moyes alietokea Everton.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment