 
  Waziri
 wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akipongezwa na Mkurugenzi  
Msaidizi wa Wanyamapori Paul Sarakikya mara baada ya kumaliza mahojiano 
 katika kituo cha BBC jijini London alipokuwa akihudhuria Mkutano wa  
Kimataifa wa Biashara Haramu ya Wanyamapori. Kulia ni Katibu wa Waziri  
Imani Nkuwi.

  Waziri
 wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kati) alipata fursa ya  
kukutana na Mwandishi wa Gazeti la Daily Mail la Nchini Uingereza Martin
 Fletcher (kulia) na kumfafanulia juu ya juhudi za serikali katika  
kupambana na ujangili nchini. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa  
Wanyamapori Paul Sarakikya.

  Waziri
 wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akihojiwa na Mtangazaji  
Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) Zawadi Machibya ambapo alipata 
 nafasi ya kuzungumzia juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika
  Vita Dhidi ya Ujangili nchini na Changamoto zinazohitaji kuungwa mkono
  na Jumuiya ya Kimataifa.

 Mwenyekiti
 wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe.  
James Lembeli (kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi wa Wanyamapori 
 Paul Sarakikya (kulia) jijini London walipohudhuria Mkutano wa 
Kimataifa wa Biashara Haramu ya Wanyamapori. Kati ni Katibu wa Waziri 
Imani  Nkuwi.Picha na Pascal Shelutete, TANAPA
0 comments:
Post a Comment