WAZIRI NYALANDU AKUTANA NA VYOMBO MBALIMBALI VYA HABARI UINGEREZA KUFAFANUA JUHUDI ZA SERIKALI KATIKA KUPAMBANA NA UJANGILI


 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akipongezwa na Mkurugenzi Msaidizi wa Wanyamapori Paul Sarakikya mara baada ya kumaliza mahojiano katika kituo cha BBC jijini London alipokuwa akihudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Biashara Haramu ya Wanyamapori. Kulia ni Katibu wa Waziri Imani Nkuwi.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu (kati) alipata fursa ya kukutana na Mwandishi wa Gazeti la Daily Mail la Nchini Uingereza Martin Fletcher (kulia) na kumfafanulia juu ya juhudi za serikali katika kupambana na ujangili nchini. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Wanyamapori Paul Sarakikya.
 Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Lazaro Nyalandu akihojiwa na Mtangazaji Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) Zawadi Machibya ambapo alipata nafasi ya kuzungumzia juhudi mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika Vita Dhidi ya Ujangili nchini na Changamoto zinazohitaji kuungwa mkono na Jumuiya ya Kimataifa.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Ardhi, Maliasili na Mazingira Mhe. James Lembeli (kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi Msaidizi wa Wanyamapori Paul Sarakikya (kulia) jijini London walipohudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Biashara Haramu ya Wanyamapori. Kati ni Katibu wa Waziri Imani Nkuwi.Picha na Pascal Shelutete, TANAPA
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment