NIGERIA KUCHUNGUZA UDHALILISHAJI KAMBINI!!

Kambi ya wakimbizi wa ndani nchini Nigeria
Nigeria inachunguza taarifa za ubakaji, usafirishaji wa watoto na udhalilishaji mwingine katika kambi za watu wanaokimbia mashambulio ya wapiganaji wa Kiislam wa kundi la Boko Haram.

Shirika la Usimamizi wa Majanga ya Kitaifa la Nigeria, Nema limeunda jopo la kuchunguza ukiukaji huo wa haki za binadamu.

Msemaji wa Nema ameiambia BBC kuwa wachunguzi watatembelea kila kambi ya watu waliokimbia makazi yao.

Watu wapatao milioni 3.2 raia wa Nigeria wameyakimbia makazi yao kuwakimbia wapiganaji wa Boko Haram kaskazini mashariki mwa Nigeria.

Uchunguzi wa shirika la Nema ni matokeo ya ripoti iliyochapishwa na Shirika la Kimataifa la Taarifa za Uchunguzi lenye makao yake Calabar Nigeria(ICIR).
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment