Akizungumza na gazeti
 hili jana akiwa njiani kuelekea Dodoma kushiriki Kikao cha Bunge la 
Katiba, Lema alisema maafisa wawili wa polisi walimfuata katika hoteli 
aliyofikia Dar es Salaam kwa lengo la kumkamata na kumpeleka makao makuu
 ya polisi. 
Lema alisema maafisa hao, ambao walikuwa 
wanatumia gari dogo, baada ya kufika hotelini hapo, waliomba aitwe na 
aliposhuka walimtaka kuandamana nao, hadi makao makuu ya polisi kwa 
mahojiano. 
“Niliwauliza nikaandeke maelezo juu ya nini, 
walijibu kifupi wao ni chombo cha dola na walisema wametumwa na viongozi
 wa juu wa polisi na hawakuwa tayari kutaja tuhuma zangu,” alisema Lema.
 
Alisema baada ya polisi hao kusisitiza kutaka kumchukua, 
aliwaomba aende chumbani kujiandaa kabla ya kuwasiliana na viongozi wa 
chama chake na familia yake. 
“Niliposhuka chini sikuwakuta 
na ndipo nikashauriana na viongozi wa chama hicho na kuamua kuondoka 
jana mchana Dar es Salaam kuelekea Dodoma. 
Hata hivyo, 
alisema Chadema leo wanatarajia kutoa tamko juu ya kauli ya Rais Jakaya 
Kikwete kuwataka wanachama wa CCM kuondoa unyonge dhidi ya wapinzani 
hasa pale wanapodaiwa kupigwa.MWANANCHI
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
                            (
                            Atom
                            )
                          

0 comments:
Post a Comment