Mkurugenzi
 wa Habari, Elimu kwa Umma na Itifaki wa Bunge Maalum la Katiba, Bw. 
Jossey Mwakasyuka (kushoto) akisisitiza jambo wakati wa semina 
iliyoandaliwa kwa ajili ya waandishi wa habari kuhusu kuimarisha 
Uandishi wa Habari za shughuli za Bunge iliyofanyika tarehe 6 Septemba, 
2014 katika Ukumbi wa African Dreams Conference mjini Dodoma. Kulia ni 
Mshauri wa mambo ya Kiufundi toka Shirika la UNDP, Bi. Anna 
Kochannesyan.
Mhariri
 Mtendaji Jamhuri Media Limited, Bw. Deodatus Balile akitoa mada mbele 
ya waandishi wa habari (hawako pichani) inayohusu Athari za Siasa katika
 uandishi wa Habari za Bunge, Madhara ya Vyombo vya habari kutumika, 
Miiko na Maadili ya kuzingatia wakati wa semina kwa ajili ya waandishi 
wa habari iliyofanyika tarehe 6 Septemba, 2014 katika Ukumbi wa African 
Dreams Conference mjini Dodoma.
Mkurugenzi
 Msaidizi Idara ya Kamati za Bunge Maalum, Bw. Athumani Hussein akitoa 
mada inayohusu Uandishi wa habari za Bunge na Siasa wenye tija kwa Taifa
 wakati wa semina iliyoandaliwa kwa ajili ya waandishi wa habari 
iliyofanyika tarehe 6 Septemba, 2014 katika Ukumbi wa African Dreams 
Conference mjini Dodoma.
Mshauri
 wa mambo ya Kiufundi toka Shirika la UNDP, Bi. Anna Kochannesyan 
akichangia mada wakati wa semina iliyoandaliwa kwa ajili ya waandishi wa
 habari iliyofanyika tarehe 6 Septemba, 2014 katika Ukumbi wa African 
Dreams Conference mjini Dodoma.
Afisa 
Habari wa Bunge Maalum la Katiba, Bw. Owen Mwandumbya akifafanua jambo 
wakati wa semina iliyoandaliwa kwa ajili ya waandishi wa habari 
iliyoandaliwa kwa ajili ya waandishi wa habari iliyofanyika tarehe 6 
Septemba, 2014 katika Ukumbi wa African Dreams Conference mjini Dodoma.
Baadhi
 ya waandishi wa habari wakisikiliza kwa makini mada zikizowasilishwa 
wakati wa semina iliyoandaliwa leo kwa ajili yao iliyofanyika tarehe 6 
Septemba, 2014 katika Ukumbi wa African Dreams Conference mjini Dodoma.
WAANDISHI
 wa habari nchini wameaaswa kuandika habari  zinazohusiana na masuala ya
 Bunge, likiwemo Bunge Maalum la Katiba kwa kuzingatia weledi na 
kujiepusha kuwa na maslahi binasfi au ya kisiasa.
Hayo 
yalisemwa leo 6 Septemba, 2014 na Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Jamhuri ,
 Deodatus Balile wakati  wa semina  kuhusu namna bora  ya kuimarisha 
uandishi wa habari za shughuli za Bunge iliyofanyika kwenye hoteli ya 
African Dreams  mjini Dodoma.
Akizungumza
 awali kabla ya kuanza kwa Semina  hiyo iliyoandaliwa na Ofisi ya Habari
 ya Bunge kwa kushirikana na Shirika la UNDP, Mkurugenzi wa Habari, 
Elimu kwa Umma na Itifaki  wa Bunge Maalum, Bw. Jossey Mwakasyuka 
amesema lengo lake ni  kuweza   kujadiliana na kubadilishana uzoefu juu 
ya uandishi wa habari hizo kwa waandishi hao ili kuweza kuandika habari 
sahihi.
Balile
  amesema hayo  wakati    akitoa mada kuhus u Athari za kisiasa katika 
uandishi wa habari wa Bunge , Madhara ya Vyombo vya  Habari kutumika, 
miiko na maadili ya kuzingatia kwenye uandishi wa habari hizo.
“Ni 
lazima kutenganisha uandishi wa habari na siasa, ikiwa kama unataka 
kuingia katika siasa basi inapaswa kuacha kazi ya uandishi wa habari,” 
alisema Balile.
Aidha,
 Balile amewataka waandishi wa habari kujiepusha kuandika   habari  
zinazohusu siasa na Bunge ambazo  zinajenga chuki katika jamii, ikiwemo 
kuiingiza hisia binafsi ama upendeleo.
“Ni 
vema  habari zinazohusu maendeleo, umoja  mshikamano na zenye kuleta 
amani zipewe kipaumbele,” alisisitiza Balile.
Aliongeza kuwa ni vema waandishi hao wakajenga tabia ya kujiendeleza 
kielimu katika fani mbalimbali ili kuweza kufanya kazi hiyo kiufasaha na
 kujiheshimu  kwani wakijiheshimu  nao wataheshimiwa,huku akiwapongeza 
baadhi yao ambao wamejiendeleza au wanajiendeleza kielimu.
Kwa 
upande wake Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Kamati za Bunge Maalum, Athuman
 Hussein, akitoa mada kuhusu Uandishi wa  Habari za Kibunge wenye Tija 
kwa Taifa amewataka waandishi hao kuweza kukumbuka mara kwa mara mambo 
ambayo yatasaidia kuongeza ufanisi katika kazi zao.  
“Unapoandika
 habari za Bunge ni lazima  uwe na uelewa wa matarajio ya wananchi  ili 
uweze kuandika habari zenye tija. Huwezi kuandika habari zenye tija  
kama hujui matarajio ya wananchi,” alisema Hussein.
Hussein aliongeza kuwa na uelewa juu ya Bunge na majukumu yake, muundo wake na mifumo yake ni jambo muhimu kwa waandishi.
0 comments:
Post a Comment