SHULE BINAFSI ZAPIGWA PINI!!

 

SERIKALI imetangaza kuzichukulia hatua kali za kinidhamu ikiwepo kuzifutia usajili shule binafsi zitakazowafukuza au kuwakaririsha wanafunzi wa kidato cha pili ambao hawatafikia wastani wa alama zilizowekwa na shule husika.

Kauli hiyo ilitolewa bungeni mjini Dodoma jana na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dkt.Shukuru Kawambwa, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) Conchestar Lwamulaza, kuhusu malalamiko ya wamiliki kuweka alama za juu za ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha pili.

Alisema walipokea malalamiko mbalimbali ya wazazi juu ya suala hilo na kwamba Serikali inakataza kutokumkaririsha darasa, kumhamisha wala kumfukuza kwani tayari Serikali kupitia kwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo alishaandika barua kwenda kwa wamiliki wa shule na mameneja kuhusiana na jambo hilo.

Alisema waraka wa 10 wa mwaka 2012 wa elimu unazuia kumfukuza mwanafunzi akiwa mwaka wa mwisho wa masomo.

Dkt. Kawambwa alisema baada ya kupokea malalamiko mbalimbali ya wazazi, Serikali inapiga marufuku suala hilo kwani wastani wa kufaulu kwa mwanafunzi wa kidato cha pili ni alama 30.

"Natoa agizo mbele ya Bunge lako Tukufu kuwa kwa wamiliki na mameneja wa shule zisizokuwa za Serikali kuanzia sasa yeyote atakayekaidi agizo hilo atachukuliwa hatua kali za kisheria," alisema Dkt.Kawabwa.

Katika hatua nyingine; Dkt. Kawambwa alisema Serikali inaendelea kijipanga ili kutekeleza agizo la Rais Jakaya Kikwete kuwa mwaka 2016 shule zote za msingi na Sekondari wanafunzi watasoma bure bila kulipa.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment